Monday, August 1, 2011

BALOZI IDD ASEMA WANANCHI WENGI WANAPENDA SEREKALI MBILI JE UMEWAULIZA HAO WANANCHI BALOZI IDD..?

Imeandikwa na Khatib Suleiman, Zanzibar; Tarehe: 1st August 2011 SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imesema wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wameonesha ukomavu na kupanuka kwa demokrasia licha ya kutokuwepo kwa kambi ya upinzani, na kusisitiza kuendelea kutumika kwa mfumo wa Serikali mbili visiwani humo.Makamu wa Pili wa Rais, Balozi Seif Ali Iddi alisema hayo wakati akiahirisha kikao cha Baraza la Wawakilishi mwishoni mwa wiki kilichokuwa kikijadili na kupitisha Bajeti ya Serikali pamoja na matumizi ya Wizara za SMZ kwa mwaka wa fedha 2011/12.Alisema demokrasia katika Baraza hilo imepanuka sana na wajumbe wameonesha ukomavu wa kuhoji na kuibana Serikali kwa mambo mbalimbali bila ya kujadili itikadi za vyama vya siasa.“Mheshimiwa Spika nimefurahishwa na jinsi wajumbe walivyokuwa wakiihoji Serikali katika mambo mbalimbali…..hali hiyo imeonesha ukomavu wa kisiasa kwa wajumbe bila ya kujadili itikadi za vyama vya siasa,” alisema Balozi.Balozi aliwaahidi wajumbe hao pamoja na wananchi kwa ujumla kwamba Serikali itafuatilia mambo yote ya msingi yalihojiwa na katika baraza hilo kwa maslahi ya taifa.
Alisema Serikali ya Awamu ya Saba chini ya Rais Dk. Ali Mohamed Shein, itakuwa makini na haitovumilia kuona uchafu ukifanyika ikiwemo wa uvunjaji wa sheria na taratibu zilizowekwa na nchi.Katika hilo, aliwataka watendaji wakuu wakiwemo mawaziri kuwa makini kusimamia utekelezaji wa majukumu yao na kamwe wasitoe nafasi kuwepo vitendo vinayorudisha nyuma imani ya wananchi kwa Serikali yao.Kuhusu muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Balozi alisema mfumo wa Serikali mbili ndiyo uliokubaliwa hadi sasa na Chama Cha Mapinduzi ambacho sera zake ndiyo zilizotumika kikatiba katika kuongoza nchi na Serikali ya Umoja wa Kitaifa.“Hili nataka kulifafanua tena, mfumo wa Serikali mbili ndiyo uliokubalika na wananchi walio wengi ambapo kwa upande wetu sisi tunatekeleza sera ya Chama Cha Mapinduzi katika mfumo wa Serikali ya umoja wa kitaifa,” alisema Balozi Idd.Aidha, alikemea baadhi ya tabia za Wazanzibari kuwatimua wenzao wa Tanzania Bara ikiwemo kuwahamisha na kuwafukuza kwa nguvu kwamba ni sehemu ya vitendo vya kibaguzi ambavyo havikubaliki.Alisema Mtanzania kwa mujibu wa Katiba, anayo haki ya kuishi sehemu yoyote ya Tanzania kama ilivyo kwa Wazanzibari kuishi sehemu yoyote katika ardhi ya Tanzania Bara bila ya kubughudhiwa.

MIMI NAKUAMBIA USITULETE MAMBO YA MAPINDUZI MAANA HAYO NDIO YALIYOUTIZA ZANZIBAR UMASIKINI NA KUWAFANYA WAZANZIBAR KUKIMBIA KWAO NA KUWA WAKIMBIZI MPAKA SASA WAZENJI KIBAO NI WAKIMBIZI KWA SABABU YA MAPINDUZI UNAYOJISIFIA WEWE ZIMWI BALOZI IDD PIA USHAWAHI KUWAULIZA WAZENJI KAMA WANAUTAKA MUUNGANO HUWO WA SEREKALI MBILI AU UNANGOJEA MPAKA WATU WAJAZANE BARABARANI KUUPINGA NDIO UJUWE KAMA HAWAUTAKI..?KAMA HUNA LA KUSEMA NYAMAZA KIMYA ULE ULUWA WAKO WAKATI KUISHA URUDI BARA HUKO KAMA NI UBAGUZI MULIANZA NYINYI BAADA YA KUONA ZNZ IMEPEWA UHURU UHASIDI UKAWAINGIA NA KUIVAMIYA MPAKA LEO ZNZ INAGARANGARA KWA AJILI YA MAPINDUZI MUSITULETE HAPA HAKUNA MAPINDUZI WALA ACHARI.

No comments:

Post a Comment