Sunday, June 17, 2012

JESHI LA KIKURIA LA KITANGANYIKA NCHINI ZANZIBAR LINAENDELE NA UKABURU WAKE KWA KUWAPINGA WAZENJI WALIO KUWA WANAKWENDA KWENYE MHADHARA DONGE BIDI KUHAIRISHWA


Waislamu waliofika katika viwanja vya Malindi baada ya kutawanywa na jeshi la polisi la kikuria huko Mahonda ambapo walikuwa wakienda Donge kwenye muhadhara ambao umebidi uhairishwe baadhi ya watu wameumizwa baada ya kupata kipigo kutoka kwa polisi wa kikuri wanao tawala zanzibar kwa mabavu toka 1964 kutoka nchi jirani tanganyika.wame wapinga wanawake pia vibaya sana  ambao ilibidi wakimbilia msikitini ili wahifadhike na polisi hao wa kikuria waliokuwa wakiwapiga pasi na huruma lakini haikuwa dawa kukimbilia msikitini maana waliwafuata humo humo msikitini na kuwapa kichapo huko huko ndani ya msikiti nakuwapinga risasi na mabomu ya machozi.HONGERA SEREKALI YA SHEIN NA SEIF SHARIFF.

Ipo wapi imani na hadhi ya wazanzibar? katika kipindi cha mwisho wa uongozi wa DR Amani Abeid Karume zanzibar ilisifika sana kwa utulivu na mpaka kuwa mfano kwa mataifa mengine ya afrika. Hii imetokana na kuonekana uchaguzi umeisha kwa salama na amani, vile vile katika hotuba ya DR Shein aliyohutubia baraza la uwakilishi wakati anaingia madarakani alisisitiza amani na utulivu iendelee zanzibar na pia alisisitiza mwezi uliopita kwa kusema “asieitakia amani zanzibar ahame”
Jioni ya leo kwa masikitiko makubwa jeshi la polisi limewazuia waumini ambao walikua wakienda katika mhadhara ambao ulikua ufanyike Donge na kusababisha majeruhi wengi sana. Jeshi la polisi liliekaa mahonda na kuzuia waumini wasipite kitendo ambacho kiliwafanya waumini hao ambao wanadai haki yao wabaki katika msikiti mkubwa wa mahonda huku wakiwasubiri viongozi (maamiri) wao waamue nini kifanyike, cha kushangaza kwamba viongozi walipowasili na kutaka kuonana na jeshi la polisi ilitoka amri kwa kiongozi wa jeshi hilo kwamba wawapige waumini ambao walikuepo hapo.
Kwa kua amri ndio ishatoka jeshi la polisi likaanza kutawanya mabomu kama ilivyo kawaida yao na kusababisha kina mama wengi kupata kichapo ambacho hastahiki kufanyiwa mwanamke,
Jambo ambalo la kusikitisha ni pale ambapo waumini walipoamua kujihami na kuamua kuingia ndani ya msikiti ili wapate usalama kwa kuamini serikali inaheshimu nyumba za ibada lakin kumbe imekua makanisa ndio yanaheshimiwa. Kwa kweli jeshi la polisi limevamia msikiti wa mahonda ambamo waumini wengi walijificha humo nakuanza kupigwa mabomu ambayo yana risasi za mipira na hatimae msikiti kuwa na kuenea damu nyingi z waislamu vile katika msikiti wa Donge nako waislamu wamepigwa ndani ya msikiti na kuumia vibaya.
Jumuiya imejaaribu kuwahudumia baadhi ya majeruhi ambao waliokuwa nao na kuwapeleka katika spitali ya ARRAHMA kwa ajili ya matibabu mpaka sasa idadi ya majeruhi haijajuilikana kwasababu kila muda imekua gari za wagonjwa zinapishana hospitalini hapo. mpaka sasa viongozi wote wa jumuiya wapo katika hali ya usalama na wamesema siku ya jumatano ndio watatoa tamko la jumuiya.

No comments:

Post a Comment