Tuesday, January 22, 2013

MTWARA NI TANGANYIKA NA WAMEGOMA GASI YAO ISIPELEKWE DAR SISI NCHI NCHI NCHI TUNAIWACHA NAKUFANYWA DAGUURO KWELI WAZANZIBAR BATATA ZA UROJO ZIMETULEMAZA



SAKATA la kupinga ujenzi wa bomba la gesi inayovunwa katika Kijiji cha Msimbati mkoani Mtwara kwenda Dar es Salaam, limechukua sura mpya baada ya maelfu ya wakazi wa Mkoa wa Mtwara kujiandikisha katika fomu maalumu kupinga mradi huo.
Tayari majina hayo yamekabidhiwa kwa Katibu wa Wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF), Magdalena Sakaya kwa ajili ya kuyawasilisha bungeni kama kielelezo halali cha wananchi hao kupinga mradi huo, ambapo utaratibu wa wananchi hao kujiorodhesha uliandaliwa na chama hicho.
Taarifa zinaeleza kuwa zaidi ya wakazi 30,000 wa Mtwara wamejiorodhesha kupinga mradi huo wa gesi.
Makabidhiano hayo yamefanyika kwenye mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Mashujaa mjini Mtwara na kuhudhuriwa na maelfu ya wananchi kutoka wilaya zote tano ya mkoa huo, ambao hawakujali mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha.
Watu wa kada mbalimbali waliliambia Mwananchi Jumapili kwamba haijawahi kutokea umati mkubwa wa watu kuhudhuria mkutano wa hadhara mkoani humo kama ilivyokuwa kwa mkutano wa jana.
Walisema kuwa idadi hiyo ya watu ni zaidi ya waliojitokeza katika maandamano ya kupinga mradi huo, yaliyofanyika Desemba 27 mwaka jana.
Majina hayo yalikabidhiwa na makatibu wa CUF wa wilaya za mkoani huo  huku mwakilishi wao Saidi Kulaga, akisema kuwa zaidi ya watu 30,000 wamejiandikisha kupinga mradi huo.
Alisema wananchi hao wanataka Serikali kujenga mitambo ya kufua umeme  mkoani humo, ili kuinua uchumi wa mikoa ya kusini.
“Kwa niaba ya wananchi hawa na mbele yao,  nakukabidhi majina na  sahihi zao, wakipinga mradi wa kusafirisha gesi kwenda Dar es Salaam. Wazee wetu waliwaondoa wanyonyaji weupe, sasa ni zamu ya vijana kuwaondoa wanyonyaji weusi,”  alisema Kulaga huku akishangiliwa na umati wa watu.
Akipokea fomu hizo, Sakaya alisema kuwa wabunge wa CUF, wamesikia kilio cha wananchi wa Mtwara na kwamba watahakikisha wanawasilisha katika Bunge lijalo.
Katika mkutano huo mabango kadhaa yalibebwa na baadhi yakisomeka: “Shemejiii gesi haitoki…: Kikwete tuachie gesi yetu.”
Kabla ya mkutano kuanza umeme ulikatika eneo hilo hali  iliyosababisha kundi la vijana kuivamia Ofisi ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), mkoani humo wakiishinikiza urudishwe, kitendo kilichowalazimu polisi kuingilia kati na kufyatua mabomu ya machozi ili kuwatawanya wananchi hao.
Wananchi waliondoka eneo la ofisi hizo na kurudi uwanja wa mkutano, ambapo baadaye na mkutano huo uliendelea kwa  amani na utulivu, huku polisi wakiwa katika tahadhari kubwa.

No comments:

Post a Comment