Sunday, February 24, 2013

AKIULIWA PADRI FBI,CIA,SCOTLAND YARD WATUWA NCHINI ZANZIBAR AKIULIWA SHEIKH HAAA NI MTU TU WAKAWAIDA!!!!!


SAIDI MWEMA SIKU YA KIYAMA UTAMUAMBIA NINI M/MUNGU WEWE..?
WAKATI kukiwa na taarifa kwamba maofisa wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) wametua nchini kwa ajili ya kufanya upelelezi wa mauaji ya Padri Evarist Mushi,wazanzibari wamejawa na huzuni kuona nchi ya tanganyika inaipakazia zanzibar ugaidi na lakumiza zaidi nikuwa sheikh wa msikiti ameuliwa na hakuna hata radio au tv iliyotangaza kuhusu tikio hili.isitoshe Jeshi la Polisi limetangaza dau la Sh10 milioni kwa atakayefichua aliyemuua padri huyo lakini jeshi hili hili la polisi limeshindwa hata kufafanuwa kwa kuliwa sheikh huyo ambaye sasa ni siku ya pili tu toka auliwe lakini hakuna hata polisi moja anaelizungumziya jambo hili kila moja anazungumzia kuhusu padri mushi tu na sio sheikh je hii kweli ni haki...?
Padri Mushi aliuawa kwa kupigwa risasi Beit el Ras nje kidogo ya mji wa Zanzibar, ambapo inadaiwa kuwa waliomuua walikuwa wamepanda pikipiki aina ya Vespa na walimfyatulia padri huyo risasi tatu akiwa ndani la gari yake.sheikh nae ameuliwa akiwa katika shamba lake alipingwa na mapanga na magaidi wasio julikana na kufaa alipokuwa akiharakishwa hospitali kutokana na kutokwa na damu nyingi alikufa ni jambo la ajabu sana haswa zanzibar nchi ndogo kama hii kukawa na magaidi hawa wa kuwauwa masheikh kwa mapanga bila ya huruma kabisa.
 Sheikh Ali Khamis Ali (65) mkazi wa Kitope Kaskazini Unguja, aliuawa jana kwa kukatwa katwa na mapanga nchini Zanzibar, baada ya magaidi wasio julikana kuvamia shambani kwake.Habari za kuaminika zilizopatikana juzi zinaeleza kuwa maofisa hao wa FBI, wako nchini na tayari na wamekutana na baadhi ya viongozi wa Serikali kwa ajili ya kuanza kazi hiyo ya kuchunguza kifo cha padri tu je cha sheikh au sheikh sio mtu...?
Chanzo chetu cha habari kimeeleza kuwa maofisa hao walikutana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi kwa ajili ya kuangalia ni namna gani watafanya shughuli zao katika upelelezi huo na toka sheikh auliwe nchimbi hajaja tena nchini zanzibar kusema kuwa hawa walio muwa sheikh pia ni magaidi na tutawasaka hakuja kabaki dar kimya nini tufahamu wananchi wa zanzibar ikiwa akiuliwa padri ni ugaidi akiuliwa sheikh kimya akiuliwa padri fbi akiuliwa sheikh kimya ni nini tafsiri ya mambo haya...?
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima alilithibitishia gazeti hili kwamba Serikali imeanza kufanya mazungumzo na mashirika mbalimbali ya upelelezi duniani kwa ajili ya kushirikiana nayo kuchunguza mauaji ya Padri Mushi, lakini akasema kuwa ni mapema mno kuyataja.
“Tumeahidi kutoa Sh10 milioni kwa mtu yeyote, atakayetoa taarifa za mauaji ya Padri Mushi, hii itakuwa kama zawadi tu.”je sheikh Ali Khamis Ali mtatowa kiasi ngani...????

No comments:

Post a Comment