Thursday, May 23, 2013

SHEHA TOMONDO AMWAGIWA TINDIKALI NCHINI ZANZIBAR

Sheha Tomondo       baada  ya kumwangiwa tindi kali sheha                                                                                                                                                                                  Sheha wa Tomondo Mohamed Omary Said amemwagiwa tindikali na mtu asiyejulikana na hivyo kupata maumivu makali sehemu ya kifua na jicho.

Sheha huyo alikimbizwa katika Hospitali ya Mnazi mmoja mjini Unguja ambapo alipatiwa matibabu ya dharura.
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mukadam Khamis anajifanya kama FBI au CIA alijidai kusema chombo kilichotumika kumwagia tindikali Sheha huyo kilipatikana eneo la tukio na kwamba polisi wamekichukua kwa kukichunguza kitaalam ili kugundua aliyekuwa akikitumia kwa kuangalia alama za vidole. swali je munavidole vyote vya rai wa nchi hii ya Zanzibar...???
Sheha huyo alimwagiwa tindikali jana usiku wakati alipotoka nje ya nyumba yake kuchota maji na ndipo jamaa huyo mwenye asira nae alipomwagia tindikali na kwamba hakuweza kumtambua ni nani.lakujiuliza je huu sio mpango mwengene wakutaka kuzusha fitina zaidi ya Wazanzibari..?? au tayari polisi wana mpango wakusingizia mtu kesi yani wanataka wafanye haya kisha waseme ni fulani ili wasukumizie kesi na kumtupa korokoroni kama walivyo msingizia yule kijana wa watu kuwa ati kamuwa padri..???

No comments:

Post a Comment