Tuesday, August 6, 2013

BORA KULA MASHELISHELI NA MUHOGO WA HALALI KULIKO MAPOCHOPOCHO NA MANONO YA HARAMU


Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa 

Wateja wa CRDB ya

Benki, Tully Esther Mwambapa akiucheza shere uislamu na 

waislamu kwa 

ujumla. akizungumza katika hafla ya kufuturisha iliyoandaliwa na 

benki hiyo kwa ajili ya 

wateja wake.je hili vazi na kuna wanume wanawake zao na hata 

kama hawana wake je 

ndio munafuturu na huku munajaza thambi katika mabuku yenu 

mana yeye yuko uchi.

Leo nitazungumzia kidogo jinsi dini yetu ya kislamu tunavyo ifanya kama mkorogo vyogo.Kumezuka mtindo hapa nchini kwetu Zanzibar kwa Mabenki, Hoteli za kitali na Viwanda vya kutengeneza vinywaji wasemavyo wao havina kilevi kufuturisha watu. Tuka tukijuwa kuwa bora ule muhongo wako wa konde iliyo yako mwenyewe kuliko kula manono ambayo pesa zake sote tunajuwa kuwa zimepatikana kwa njia ya haramu kwahiyo hauli manono unakula moto. Hili suala la kufutarisha sasa limekuwa fashion hasa hapa nchini kwetu Zanzibar, na mimi nimekuwa concern nalo sana lakini katika mtazamo kuwa ‘kwa kiasi gani uislamu unazidi kufujwa na kuharibiwa na waislamu wenyewe’. Hilo ndio ninaloliamini, na ndivyo lilivyo. Mifano, ni mingi tu kuwa uislamu tunauharibu wenyewe.pia napenda kuwajulisha watu kuwa  umealikwa iftar zote hizo za Kibenki,za Kihoteli sio lazima kwenda hata moja sisi ni waislamu lazima tuziweze nafsi zetu na nyoyo zetu na roho zetu sio kila tunapo alikwa sisi tumo tu kama makumbi. CRDB imealika Wazanzibari iftar, Ramadhan ya tatu; meneja wao mwanamke alivaa nguo kama ankwenda kucheza disco Bwawani, backless, sleeveless/nguo haina mikono, haina stara watu wanafuturu nae hiyo saumu yako uliyo saumu siku nzima mpaka unamaliza ndio unaitia katika kapu bovu— hii ni kutuvunjia heshima waislamu. Waislamu tunajidhalilisha kwa kokwa ya tende au kikombe cha uji, na watu amabo sio mutatahirina ndio wanaokuw ambele yetu,na sisi tumo tu, tumetiwa shemere.                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                              Uislamu hasa Zanzibar tunaendelea kuuharibu wenyewe: angalia check list ifuatayo:
1) Madrassa zetu nyingi zimegeuzwa kama vikundi vya sanaa, tunapiga magitaa, ganun, na violin, tunakwenda kuburudisha katika sherehe za harusi, tunarekodi katika mahoteli makubwa makubwa ya kitalii video kama muziki wa Bongo flava  na tunaona sifa, na tunaona ndio dini yenyewe hiyo, ndio imani yenyewe na ni ibada.                             2)Angalia tunavyopiga music ndani ya misikiti, eti watu wana (‘dhikir’) sisi tunamfuata mtume Muhammed S.A.W. je yeye alipiga muziki kama tunavyo piga sisi..? kama hajafanyapo sisi tumeyapata wapi..? tena kwa mabomba makali na sauti za kuimba. kwani kumdhikir Allah lazima uimbe, na lazima mabomba..? mpaka ukere watu, wa mtaa mzima..? Anayepinga haya, apite pale karibu na Amani, unaitwa msikiti ngamia — pale ni kelele 24 hours: imani gani ile ya kijinga na kishirikina, na ofisi ya mufti imekaa tu, na waislamu wamekaa wanaona uislamu unaharibiwa, na wanabaki kucheka – ile sio kufanya ibada ila ni ushirikina na upotofu wa darja ya juu katika uislamu. Hivi kweli hakuna muislamu anayeona kuwa vile sivyo...?
Tumebaki kuwa waislamu wa kula sambusa, keki, vileja,halua na kualikwa hizo futari za kitaghuti.                     Juzi nilisema kuwa hao wanaotulaika futari ndio wamewaweka masheikh wetu wa Uamsho na wengine wengi wa kizanzibari, waislamu ndani JELA bila ya kosa lolote –kisha leo hao hao wanatualika futari na sisi unakwenda wao hao walio waeka masheikh wetu JELA  wamejificha katika kivuli cha iftari na sisi tumo tunajumuika nao.
Waislamu tumeuchukua ujinga, na kuufanya kuwa ndio ustaarabu, tunajua kuimba, kucheza dansi misikitini katika nyumba ya Mwenyezi Mungu, lakini quran hatuijui kuisoma hata kidogo wachilia mbali kuitafsiri au tafsiri yake hatuijuwi kabisa; siku hizi vikundi vingi vya ‘kasida’ (ngoma) vimeanzishwa misikitini – hapo utakuta watoto wari au mijari iliyo iva kweli kweli ,au majibaba wanafanya mazoezi ati haya yote ni mambo mabaya – na huwa haichukuwi muda utasikia wanatiana mimba, au wanaume kwa wanaume wanafanyana kama kaumu luti n.k. je tunakwenda wapi waislamu..??
Kuna chuo kimoja (madrassa) eti wandhikiri mpaka saa tano usiku!!!!!!! na ikifika saa nne wanazima taa Astahafiru Allah– wake kwa waume humo ndani kisha munazima taa:..? mimi niliuliza siku moja  je wazee wa mtaa wako wapi,..? wazee wa watoto hawa wa kike na wakiume wako wapi;..? je, hawa watoto hawasomi skuli...?  n.k.  average kwa mwezi wanafunzi kama wanne mpaka watano wanatiwa mimba kila mwezi hapo  sisi  tuendelee kula sambusa, visheti,  bajia, halua, keki , na iftari na kuacha misingi mikuu ya imani, dini na hushui — dini nchi mwetu Zanzibar tunaiharibu wenyewe, na inazidi kuyoyoma.Tuendelee kucheza dansi msikitini, n halua kwa wingi!!!!!!

No comments:

Post a Comment