Tuesday, February 11, 2014

BALOZI MDOGO WA NCHI YA TANGANYIKA MISAADA MINGAPI YA MAMILLIONI ULIYO KULA...? HAYAKUWAFIKIA WAZANZIBARI


HUYU SIO MAKAMO WA RAISI HUYU NI BALOZI WA KUPOKEA MISAADA YA WAZANZIBARI WANAO KUFA KWA JELI ZA MELI KISHA YEYE NA WAKEREKETWA WENZAKE WANAKULA PESA HIZO ZA MISAADA.

Sawa, mengine ni kudra ya Mwenyezi Mungu; lakini na binadamu anatakiwa kupanga mambo yake kimaisha ya kila siku.
Kipindi kifupi sana tumeona nchi yetu ya Zanzibar imekumbwa na maafa ya kila aina — kuzama kwa meli, dharba za meli, upepo na mvua kubwa (mafuriko). Kati ya yote haya, na mengine Idara ya Maafa haikuonekana mbele ya umma wa Wazanzibari kabisa hata kujisogeza mbele na kutoa ushauri au kusaidia au angalau kuonyesha ubinadamu.
1. ) Jana upepo mkubwa umeharibu nyumba zaidi ya 67 huko eneno la Nungwi, hakuna hata ‘salam’ au response kutoka Idara ya Maafa, ipo chini ya ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Balozi mdogo wa Tanganyika.
2. Upepo wa Pemba, umeezua nyumba nyingi na ushei (no response) ila watu binafsi mara hii wamejitutumua kidogo na kusaidia.  Idara ya Maafa imelala chalii — inasubiri wapelekewa michango ya misaada na kuitumiya wao na kula tu.
3. Imezama MV Spice islander — hakuna response ila tuliona vikosi na bunduki na kutisha watu na kuwaibia wahanga malizao,thahabu zao,N.K   mbaya zaidi, misaada ya mabilioni haikuwafikia wananchi kabisa nao tulosikia atii yamewafikia atii wamepewa liki moja hawakukoseya wabongo laki si pesa. (VP2 ofisi Balozi ndogo wa Tanganyika ni ulaji tu mbele kwa mbele).pesa zote za misaada kazitaifisha yeye na wakereketwa wake.
4. Imezama MV Skagit — kadhalika, hatukuona Idara ya Maafa wala Mazingira wala nani na nani — ila tumeona misaada ikitolewa na haikuwafikia wananchi walioathirika — pesa zimeliwa na hakuna maelezo/si kwa wawakilishi wala wabunge wala nani na nani — ni ulajii tu na  mbele kwa mbele.
5. Kuna kipindi tulikumbw na mafuriko, pia waliopewa magodoro ni wale wanojulikana ni CCM kama sio CCM mtajiji sasa hayo mapinduzi yalikuja kuondowa ubaguzi yako wapi mbona huo ubaguzi ndio kwanza unashamiri na kuvaa njuga.....? (kwa ushahid upo!), wengine mkatafute……!
Pale kuna Mkurugenzi anaitwa Ali Juma, huyu anachokijua ni U-CCM tu, hata Zanzibar yote igharik hajui afanye nini wala hana habari — yeye anajifanya CCM sana na mkereketwa wa nguvu: heee wewe jamaa yangu, utakuwa CCM kweli wewe kuliko Mzee Moyo au Mzee Aboud Jumbe na Ramadhan Haji Faki (waulize wamefanywa NINI na hiyo CCM unayo ikingia kifua na kujitutumuwa nayo);  Mzee Moyo anasalimika kidogo nadhani Kikwete anamuwekea ‘ngao’ kwa mbaaali, anajua angalau ihsani aliyomfanyia ya kumpatia Urais. Mwenzake Shein hana ihsani hiyo.
CCM Oyeeee, CCM daima Oyeeee, CCM ushindi Laizma Oyeee…..mukitaka msitake ni CCM tu Oyeeee mkibisha sana tunaita majeshi na polisi wawauwe Oyeeeee na katiba mlijidai kuipinga na kuipiga moto sasa wenyewe mumekubali na kuka na sisi kuitengeneza katiba  Oyeeeee mnafikiri ni katiba ya TANGANYIKA NA ZANZIBAR lakini sisi nia yetu ni kuwa hii katiba misho wake ndio itakuwa katiba ya nchi na kikatiba chenu cha Zanzibar kitabaki kuwa kama gazeti la nipashe Oyeeeeee hakuna cha mkataba muliotaka wala mkutubu na iko siku mutatubu na katiba hii mpya ni serikali mbili (kama tulivyo na kuelekea moja) Oyeeeeee.

Yalipotokea maafa ya upepo kule Pemba, Idara hii ilinuna sana na waliuliza kwa nini watu binafsi wanatoa misaada moja kwa moja, walitaka ipelekwe kwao Idara ya Maafa, then, eti wao ndio waipeleke kwa wananchi. Wallah wangaliiba hata magunia ya mchele wa mapembe na yale magodoro. Watu binafsi wamefanya jambo zuri mara hii na wanastahiki pongezi na sifa endeleani hiyo hivyo mukitaka kuisaidia pemba au unguja basi hawa majinamizi musiwambiye kabisa.
Na anayetaka kusaidia Nungwi, afanye kama hivyo, vyenginevyo, hawa SMZ na Idara yao ya maafa watachukua mpaka pakti ya chumvi ya sh 300/= hawa hawatosheki wala hawashibi maisha. Pale VP 2 Balozi mdogo wa Tanganyika office watu wametajirika kwa maafa na sherehe za mapinduzi. na Ujenzi wa mnara….? hakuna hesabu, hakuna auditor etc.

No comments:

Post a Comment