Monday, February 10, 2014

CUF HAINA UWEZO YA KUWAPA WAZANZIBARI MAMLAKA KAMILI NI UAMSHO TU YENYE UWEZO HUU KWA UWEZO WA M.MUNGU


TUACHIWEE TUPUMUWEE TUACHIWEE TUPUMUWEE TUACHIWEEE TUPUMUWEEEEE

Nimeona na kusoma kutoka maandiko mbali mbali yanayozungumzia juu ya kuvurugwa  na ukiritibwa uliyo fanywa kwanye uchaguzi wa Kiembesamaki,Bububu, n.k na CCM chama cha Wauwaji. Nimesoma vile vile matamshi ya viongozi wa CUF wasio juwa usiku wala mchana wasio soma wakati wala wasio juwa kuja na mbinu mpya. kwa mfano Maalim Seif alipohutubia mkutano wa viongozi Pemba, na Mkurugenzi atii  wa haki za binadamu Salum Dimani kuhusu sakata zima la uchaguzi huo yaguujuuuuuuu.
Habu tujiulize yaliotokea Kiembesamaki  ndio mara ya kwanza kutokea hapa nchini kwetu Zanzibar....? kama hamulijuwi jibu mimi nitawapa jibu ni hapana yashatokea mara chungu mzima sio tu katika changuzi za jimbo bali hata katika uchanguzi mkuu wa Uraisi yashatokea kuanzia wakati wa Maalim seif na Komando wa Udongo mpaka sasa ni Maalim na Maacheni yumo kuwafunga Wazanzibari maacheni ya Ukoloni Mweusi Tanganyika. Sote tunajuwa kuwa si mageni kwa sababu yanatokea katika chaguzi zote hasa za Unguja.
Tumeona uchaguzi wa Bububu na chaguzi zote tokea 1995 mikakati ni ile ile na matokeo ni yale yale.
Nafikiri ni wakati sasa kwa wananchi wa Zanzibar kukaa na kujiuliza mambo haya yataendelea mpaka lini...? Pia niwakati wakujiuliza hivi kweli dawa ya kuingowa CCM na wahafidhina wake wanao wanyonya,wauwaji,kuwatia maradhi,vilema,umasikini na ufukara Wazanzibari ni CUF.....? kama hamulijuwi jawabu nitawapa tena sio CUF SIO SIO SIO CUF haiweze kuingowa CCM hapa Zanzibar ngoooo ngooooo nakama hamuwamini endeleani kukimbiza mwenge wa CUF mutaona kama hata nyinyi vijana leo hamtajikuta mushakuwa mababu na bado muna CUF yenu mnasubiri uchangu baada ya changuzi hakuna liwalo. kwa nini nikasema hivyo nikuwa toka Maalim anze kugombea Uraisi hivi kweli ashawahi kushindwa kikura tusema ile haki hajawahi kushindwa hata changuzi moja lakini kwa nini hawi raisi....? ni kuwa huu ndio mpango mzima kuwa asiwe raisi na nyinyi mtapiga kura mkipiga tena na atashinda sio kuwa hashindi la atashinda lakini hawa raisi hapa.
 Angalia lile raisi bagbow liliposhindwa na kukata kuondoka watu wake walifanya nini...? wiki mbili tu mambo kwisha sasa yuko jela ya kimataifa huko ulaya uholanzi raisi wa madagasca alipo shindwa na yule mbwamdogo nae akagoma kuondoka ikulu angalia watu wake walifanya nini wiki tu mambo kwisha hapa Maalim anashinda kisha anakuja nje anasema tulieni tulieni muacheni yeye awe raisi maara hii sisi tutashinda tu tena uchanguzi ujao kisha nitakuwa raisi kama ndio hivyo kwa nini basi tukapiga kura Maalim simugelitangaza tu kuwa huyu ndio raisi wa sasa baada ya miaka mitno mimi nitakuwa raisi basi lakini wapi shengesha shengesha kisha hamna kitu. nchi zote za duniani zimejarubu kufanya ukiritibwa wa kuwa baba kama waziri akiondoka basi mwanawe awe waziri,baba akiwa mbunge basi akindoka mwanae awe mbunge baba akiwa spika basi akiondeka mwanae awe spika baba akiwa jenerel basi akindoka mwanae awe jenerel baba akiwa jaji mkuu akindoka basi mwanae awe jaji mkuu baba akiwa raisi basi akindoka mwanae awe raisi nchi nyingi zimejaribu na zimefeli hapa kwetu Zanzibar je zimefeli mbinu hizi....?
 Habu jiulizeni kuna nani hebu angaliyeni katika uwakishi,ubunge,polisi,majeshi kuna watoto wa nani kama sio wa hawa wawakilishi,wabunge,waspika,wajaji,wa raisi . kisha CCM ikisimama kwenye kiriri waarabu hivi waarabu vile wanaleta ukoloni baba akimaliza Ufalme mwana anachukuwa je wao CCM WANAFANYA NINI SINDIO YALE YALE Wazanzibari sisi wapumbavu tunapiga makofi wewe mwanao anakula unga wa madawa ya kulevya yanayoletwa na watoto wa hao hao wa Viongozi wao watoto wao wako ulaya wanasoma kisha wanarudi hapa wanakuwa kama baba zao mbunge,muwakilishi,jaji mkuu,raisi kisha anakupa zile zile kasumba za uwarabu na unyamwezi kama alivyo fanya baba yake kisha yeye mtoto wake ulaya anasoma wako yuko anauza batata za urojo huyo ndio kajaliwa bayaa zaidi anakuwa mwizi au mlaa ungaa kisha kwenye mikutono wewe unapiga kofi una ujinga wa kiasi ngani katika akili zako hata ukashindwa kufikiri....? nionyeshini kiongozi moja tu ambaya ana nyumba moja tu ...? 
Hakuna wote wanashindana kwa kujenga makasiri utafikiri hawafi na kuyawacha hapa hapa lakini mpaka leo familia za kizanzibari baba nyumba ya kupanga watoto wanalala ukumbina,chakula ndio allah ndio ajuwe wapi tunakipata watoto wa viongozi wanaponda pesa tu.kisha munambIwa Zanzibar ni nchi masiki mnapiga kofi tu na vigeregere mpaka lini...? Hivi kweli hakuna njia ya kuweza kupambana nayo na kuyakomesha MAMBO HAYA NA UKIRITIBWA HUU...? Au kwa sababu bado hatujaungana na kuweza kupambana nayo tu mambo haya...?
Haya ndio mambo muhimu ambayo yanatufanya Wazanzibari kwa upande mmoja tuuchukia muungano feki na kwa upande wa pili viongozi wa CCM kung’ang’ania muungano feki kwa sababu ndio unaowapa nguvu na uwezo wa kufanya wanayo yataka maana wanajuwa wazi kuwa mdaa unayoyoma habu niwakumbushe kidogo wakati wa Uamsho ili kuwaa hawalali maana walijuwa kuwa tonge inatoka mdomoni. Sisi Wazanzibari sio kama sote tunataka kuwa Viongozi laa hashaa lakini hao wanao kuwa Viongozi kwa nini hawafanya kazi zao wao ni kuiba tu na kujitajirisha kisha wanakuja kundanganya watu Zanzibar ni nchi masikini kama Zanzibar ni nchi masikini mbona hutaki kujiuzulu katika cheo ulicho nacho...? sio kweli Zanzibar sio nchi masikini ila Viongozi hawa sio Viongozi hawa ni maruhani yaliyo ekwa na MFALME MWEUSI TANGANYIKA yatunyonye na kunufaisha wao na wake zao na watoto wao na bwana wa MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA basi muliobaki nchi hii masikini mpaka lini...?
Tanganyika na Zanzibar  ni moja katika nchi 65 wanachama wa Mpango wa Uendeshaji Shughuli za Serikali kwa Uwazi(Open Government Partnership) au GOP ulioanzishwa 2011 zikiwemo Marekani na Brazil. Ili nchi iwe mwanachama wa mpango huo kuna mambo ambayo lazima uyatimize na yaonekane kwa vitendo, ikiwa ni pamoja na democracy kamili kwa wananchi wake. Angalia nukuu hii ambayo imo katika Open Government Declaration:
As members of the Open Government Partnership, committed to the principles enshrined in the Universal Declaration of Human Rights, the UN Convention against Corruption, and other applicable international instruments related to human rights and good governance:
Sasa inakuaje mambo kama haya yanatokea mchana kweupe katika nchi ambayo imejicommit katika umoja kama huu.....? kuanzia changuzi za mwaka 1995 mpaka huu wa mwisho kuanzia wa raisi na hata wa majimbo ni watu wangapi washauliwa ndio democrasi hiyo....? wangapi washatiwa ulimavu ndio democrasi hiyo...? mara ngapi Maalim kshinda mbona hajawa raisi ndio democrasi hiyo.....? yagujuuuu kaeni tu mkila batata za urojo. Serikali ya Tanganyika inajua kila kinacho fanyika hapa nchini Zanzibar wanatoa baraka zote yafanyike kwa manufaa yao kwani hili ndio koloni lao walilo nalo toka 1964 walipogaiwa na Mzee Karume.
Nawashauri Wazanzibari wakusanye ushahidi wa vitendo vyote vilivyotokea; kwa mfano video zinazoonyesha watu wanapelekwa kwa magari kutoka maeneo yasiohusika kwanda kupiga kura video za watu kupigwa na polisi na waalio uliwa na polisi au majeshi na hata walio uliwa na watu wasio julikana,na orodha ya watu walioahidiwa kulipwa Tsh20,000 baada ya kupiga kura nk. Wapeleke ushahidi huu kwa OGP Steering Committee pamoja na nakala kwa rais Kikwete wa nchi ya Tanganyika. Na vile vile wafungue kesi mahakamani ya kimataifa kupinga matokeo ya uchaguzi na wawasilishe ushahidi wote juu ya uovu wote uliofanyika katika changuzi zote kuanzia 1995 mapaka huu wa juzi.
Na wananchi wasimame pamoja kupinga dhulma hii na dhulma wafinyiwao Masheikh kule jela kama walivyosimama kuitetea Zanzibar katika mchakato wa katiba mpya. Kukaa kimya ni kuipa matumaini CCM wauwaji katika uchaguzi wa 2015, kuwa hakuna tabu mambo yao yanakwenda watakavyo kwa hiyo wanajuwa watafanya vile vile na zaidi katika uchanguzi wa 2015 kama hamukisamama sasa hivi na Masheikh kutolewa jela basi sahauni kabisa kabisa mamlaka kamili ya nchi yetu ya Zanzibar hayatakuja ngooo ngooo kama kweli mnataka mamlaka kamili ya nchi hii yetu ya Zanzibar basi lazima tusimame kwa sote mpaka Masheikh watolewe kule jela.Bila ya wale Masheikh hakuna mamlaka wa mumlaka hapa CUF haina lake CUF ishakuwa CCM B mambo wanayo yafanya katika mikutano yao ndio yale yale ya CCM lipi jipya taarabu wanaume wanawake kukatika viuno ndio kudai nchi huko hahahahahaha mnachekesha nchi hii haipatikani kwa taarabu na ngojeya uchanguzi ujao ahh yakhee tusubiri uchanguzi ujao tutashinda tu yagujuuu hakuna lolote uchanguzi utapigwa kura zitaisabiwa Maalim atashinda kutangazwa atatangwazwa huyo kishein chao basi Maalim atakuja tena nje ya bwawani tulein tulieni muacheni amalize miaka ya mitano kisha mimi nitashida ndio yale yale hakuna jipya kama hamuamina ngojeni mtanao wenyewe.
Mimi naamini Viongozi wa Zanzibar hawana ujuzi,huruma,wala maendeleo kwa wananchi wake wao ni mabavu tu lazima ashendi kwa kuwa ni mtoto wa karume lazima ashindi kwa kuwa ni mtoto wa abuu jahal wa Zanzibar borafya lazima ashinde kwa kuwa na mtoto wa vuai,kombo,jecha,pandu, nk lakini sio kuwa ashinde ataleta maendeleo laaa ila maendeleo yake ni kujitajirisha zaidi na familia yake na kutunza mali za wizi alizo ibaa baba yake zisichukuliwe haya ndio maendeleo yao. hawa wapi wananchi uhuru wa kweli kabisa kisiasa kuchanguwa kiongozi hapa nchini Zanzibar wamtakae ambaye wao wananchi wanao atawaletea maendeleo hilo halipo hapa Zanzibar wanachotumia ni mabavu tu, na mabavu yana siku na kikomo chake. yuko wapi Husni Mabarouk...? yuko wapi Iddi Amini...? yuko wapi Saleh...? yuko wapi Gaddafi.....? na wengine wengi tu kina Savimbi,Kabila, N.K.                                                                            
kila mara CCM Wauwaji wana fanya ufokonyoko wao na ikiritimbwa kimya kimya CUF ni kukusanya watu kibanda maita au mchangani malinda na kulalamika tu kama mwanamke hawara aliyekimbiwa bwana hawana mishion mpya kuwa jamaa tushaibiwa mara ya kwanza hii sasa mara ya pili tufanye nini hivi kweli ushawahi kusikia mtu akaumwa na nyoka mara kumi.....? hata kipofu haumwi na nyoka mara mbili lakini wapi CUF wanaumwa wakiumwa na nyoka yule yelu na wao ni hawa tusubiri mwakani tusubiri mwakani yagujuuu Wazanzibari nyote kaeni mkijuwa kuwa kama kweli munataka mamlaka kami ya nchi hii yetu ya Zanzibar ni Uamsho tu ndio njia ya kupata mamlaka kamili ikiwa ni wakweli ndani ya nyoyo zenu kuwa munataka mamlaka kamili laa kama mnataka kucheza msiwe,kibao kata,mduwara na taarabu basi sawa CUF ndicho hasa chama cha haya bila ya shaka mamlaka kamili ni UAMSHO TU UAMSHO TU UAMSHO TU  maana CCM wanaona kama wana haki ya kufanya lolote kwa sababu watu wamekaa kimya CUF imekaa kimya kimya kila ikibiwa kimya.
Ili kuepukana na matatizo haya, wajumbe wanaokwenda kwenye bunge la katiba wasikubali kupitisha kifungu chochote kama hakitoi mamlaka kamili kwa Zanzibar kuamua mambo yake yenyewe ikiwemo kuchagua viongozi wanaowataka. Bila ya kuwa na Zanzibar yenye mamlaka kamili mambo haya yataendelea milele na milele MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA ashamuamrisha kicheni kutia muakilishi wa ............ mnajuwa wenyewe na toka huko nyuma hatukuwa na muakilishi kama huyu lakini leo yumo basi ndio hivyo tena moja wawili watatu tahamaki ni wanyaturu watu ndani ya baraza la wawakilishi. UAMSHO NDIO WENYE UWEZO WA WAKUWAPA WAZANZIBARI MAMLA KAMILI NA MAENDELEO WALIO BAKI WOTE WANAGANGA NJAA TU.

No comments:

Post a Comment