Friday, February 7, 2014

KUTOWA NI MOYO SIO UTAJIRI

Ambulance
Jumuiya ya Zanzibar Welfare Association nchini Uingereza inawaomba kila mwenye uwezo wa kuchangia gharama za usafirishaji gari la kusafirishia wagonjwa kutoka London kuelekea nchini Zanzibar, Gari hilo ambalo litapelekwa Hospital ya Chake Chake Pemba kitengo cha Watoto linatarajiwa kuondoka UK mara tu gharama za usafirishaji zitakapopatika, nazo ni Jumla ya £1200.
Kwa yule ambae atakuwa na uwezo na Moyo wa kuchangia anaweza kutoa mchango wake kupitia Paypal ya Mzalendo.net na kuandika kumbukumbu Ambulance ama kwa wale waliopo UK wanaweza kuwasiliana na Mwenyekiti ZAWA UK Hassan M Khamis nambari ya simu 07588550153.
Ahsanteni.

No comments:

Post a Comment