Saturday, August 23, 2014

WAZANZIBAR UMEFIKA MDAA WA KUMG'OAA MADARAKANI SHEIN KWA MAADAMANO MAKUBWA HANA HAKI YA KUBAKI MADARAKANI HATA SECONDE MOJA

KULAWITIWA KWA MASHEIKH NA WAZANZIBARI WALIO TEKWA NYARA NA JESHI LA MAKABURU WEUSI LA KUTOKA KWA MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA WAKULAUMIWA KUHUSU HILI  SHEIN..


“Mheshimiwa tunalazimishwa kutoa maelezo wanayoyataka wao, wanatuingilia kinyume cha maumbile, wanaingiza majiti, chupa, wengine wanavuja nyuma, kama unaweza hakimu twende faragha nikakuonyeshe”
“Askari ameniingilia kisha akaniingiza jiti mpaka likakatika, kungekuwa na sehemu ningekuonyesha, Jeshi la Polisi la kwanza kuvunja sheria, waliofanya madhila haya wanawatukanisha Watanganyika na kufanya waonekane wabaya”ni moja katika wazanzibari akieleza mahakamani.
Umeshawahi kumuona Ngo’mbe akimuingizia Ng’ombe mwenzake jiti katika sehemu za siri..?? Watu wanadhalilishwa jamaniiii.Watu wanaingiziwa!!! Haki zao ziko wapi..?? Ndio watu wanavyohojiwa hivi..?? Hizi ndio faida za Muungano ee!!!!!!
Watu wanachukuliwa tu kinyemele nyemela, kisha mambo wanayoenda kufanyiwa hata hayasemeki. Serekali yetu ipo, imekaa tu ndio Muungano huo ndio Muungano huo eebooo. Muungano wa kutiana majiti na chupa mpaka wakakojoa damu na kuvuja kama Kistula. Duuuh!!
TUMEZISIKIA MALALAMIKO kutoka Mahakamani ya Mkoloni Mweusi Tanganyika Mashekh wetu wakilalamika kuhusu vitendo vya ushenzi wanavyofanyiwa na askari wa nchi ya Tanganyika, vinavyoungwa mkono na viongozi wa CCM na serikali ya Zanzibar.
Itakumbukwa wakati Samuel Sitta na Samia Suluhu walipoleta rasimu nchini Zanzibar, watu walipopata nafasi ya kuchangia, na kuchambua kwa kutoa maoni Sheikh Farid, aliichana rasimu ile, hadharani.
Samia Suluhu alisema waliyochana rasimu ile si Masheikh bali ni wahuni. Kinachotokea sasa dhidi ya Masheikh wetu, ni mkakati maalum uliopangwa na Serikali ya Zanzibar na Tanganyika Mkoloni Mweusi wa kuwaadhibu, kuwadhalilisha na kuwatesa. Wanalipa kisasi.
Katika awamu zote za Serikali zilizotawala nchini Zanzibar, hii awamu ya saba ya Shein, imefurutu adda kwa ukatili dhidi ya raia wake, ukatili dhidi ya uislamu.
Shein mbona haonekani kuwa ni kiongozi wa Zanzibar, haonekani kuwa na imani wala huruma wala mapenzi kwa Wazanzibari, anaowaongozo…kweli huyu ni ..... au ADUI wa Wazanzibari.....??
Hivyo Shein tumuhesabu vipi...?? Mbona anaizamisha nchi ya Zanzibar, au ndiyo anatekeleza jukumu na kazi aliyotumwa kutoka kwa MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA...?? Sijui kuhusu sheria na taratibu za uchaguzi za nchi ya Zanzibar, zinasemaje.
Mtu ambaye sheria haimruhusu kupiga kura nchini Zanzibar, inakuwaje yeye akaweza kupigiwa kura na kuwa rais wa nchi ya Zanzibar, ilhali yeye mwenyewe hawezi kupiga kura yake ya kujichagua au kumchagua mwingine. Mtu huyo kweli atakuwa na imani ya waliyomchagua...??
Haya yanayotokea sasa dhidi ya Masheikh na watu wengine, bila ya kutafuna ulimi yana Baraka kwa asilimia mia moja za Shein akiwa shauri moja na Balozi Seif Ali Iddi na kundi zima la akina Samia Suluhu na viongozi wa nchi ya Tanganyika Mkoloni Mweusi kupitia mwenvuli wa Muungano Feki.
Sijui watu wanafuatilia kwa kiasi gani kauli za Shein. Kuna siku kwa shikio langu nilimsikia akisema kuwa yeye hawezi kupingana na matakwa ya Kikwete na Mkapa:
Anasema: “Mimi nimefanyakazi kama Makamu wa Rais kwa miaka mitano na Mkapa…nimefanyakazi nikiwa Makamu wa rais na Kikwete…nawaheshimu nawaogopa na niko pamoja nao katika suala la chama chetu kuhusu mfumo wa Muungano,” eti huyo ndiyo ........ wa watu wa nchi ya Zanzibar, asilimia 60 wanaotaka Muungano wa Mkataba.
......... huyu huyu, Shein ndiye aliyesema hadharani kuwa yeye haitambui ile ‘Kamati ya Maridhiano’ inayoongozwa na Mzee Hassan Nassor Moyo. Huyu kweli anafaa kuwa kiongozi kwa kuwaongoza Wazanzibari. Sasa ni wakati mwafaka wa watu kutafakari.
Tangu siku aliyokaa madarakani watu wamekuwa wakisumbuliwa kwa kukamatwa ovyo-ovyo hasa Masheikh, Wapemba na wapinzani, kwa kuwekwa ndani kwa kesi za kubambikiziwa uongo.
Kiongozi wa nchi aliyekula kiapo cha kuitumikia nchi ya Zanzibar na raia wote wa nchi ya Zanzibar, hivi kweli ndiyo anawalinda na kuwatumikia. Shein, bila kumchambua sana ana chuki ndani ya moyo wake dhidi ya Wazanzibari.
Moja kwa moja namuunganisha na kauli za Kikwete, kuhusu ubaguzi dhidi ya Wapemba. Pia namuunganisha na kauli ya Lukuvi, dhidi ya Uislamu ndani ya Zanzibar. Na juhudi za viongozi wa aina hiyo kuhusu kuindoa nchi ya Zanzibar, ndani ya Dunia utafikiri wao ndio walio iyumba hii nchi ya Zanzibar.
Shein si kiongozi wa kumpa muda wa kuendelea kuwa ..... wa Zanzibar. Umefika wakati wa kumg’oa madarakani kwa maadamano makubwa.
Laiti kama ungekuwepo ushujaa kwa vijana wa nchi ya Zanzibar, ni kufanya kama walivyofanya wa Egypt, (Misri) walipoamua kumg’oa madaraka Hosni Mubarak kwa maadamano ya Tahrir Square. Wiki mbili tu, alifunga virago.
Kama bado watu wanakhofu ya kufa, kiama kitashuka unyanyasaji wa raia wa nchi ya Zanzibar, chini ya akina Kikwete, Shein, Dk Bilal, Mkapa, Ali Hassan Mwinyi, Nahodha, Lukuvi, Wassira, Kinana Samia, Vuai Ali Vuai, Uso wa sokwe na wengineo.
Umefika muda kwa raia wa nchi ya Zanzibar, kutafakari na kuachana na utegemezi wa vyama vya siasa, kuanza kutengeneza mtandao wa kuratibu maandamano endelevu kwa watu wa rika zote wa nchi ya Zanzibar, wanaume kwa wanawake na walemavu, kumg’oa madarakani Rais Feki wa Zanzibar, kwa sababu yanayotendeka ya kushikwa watu,kubambikiwa kesi watu,na hili sasa la kulawitiwa Wazanzibari katika jela ya Mkoloni Mweusi Tanganyika yanabaraka zake Shein. Hawatendei haki kabisa Wazanzibari.
Hayo ndiyo maoni yangu, ndiyo ninavyoona na si dhani kuwa kuna njia mbadala kwani juhudi za kuleta mshikamano, ili Wazanzibari waishi kwa furaha, waishi kwa kupendana, viongozi waliyoko madarani huanzisha chokochoko na uonevu bila sababu.
Watu wamechoka na uonevu wa CCM wa kila siku.....

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO HAITAKUFA SIKU HIYO.

No comments:

Post a Comment