Friday, May 29, 2015

MAALIM SEIF SHARIFF HAMAD ACHUKUWA FOMU YA KUGOMBEA URAISI NCHINI ZANZIBAR ASEMA USHINDI WAKE HAUTACHEZEWA NA MTU. ((CCM WAHARA WAKIJIPAKA))

Katibu Mkuu wa CUF ambaye ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar,  Maalim Seif Sharif Hamad akionyesha fomu za kuwania nafasi ya urais wa kisiwa hicho kupitia chama hicho baada ya kukabidhiwa na Katibu wa chama hicho wa Wilaya ya Magharibi,  Saleh Muhammed Saleh.  Kulia ni  Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Duni Haji
Nchini Zanzibar. Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad jana alichukua fomu ya kuomba kuteuliwa na chama hicho kugombea urais wa nchi ya Zanzibar kwa mara ya tano huku akisema ushindi wake hautachezewa na mtu.
Mara ya kwanza Maalim Seif Shariff Hamad aliwania urais wa nchi ya Zanzibar mwaka 1995 na amekuwa akifanya hivyo katika chaguzi zilizofuatia na kuporwa ushindi wake na sasa anawania tena kuingia Ikulu Oktoba. Baada ya kuchukua fomu katika ofisi za chama hicho zilizopo Bububu jana, Maalim Seif Shariff Hamad alisema ataheshimu matokeo ya urais endapo uchaguzi utakuwa huru na wa haki. Maalim Seif Sharrif Hamad ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa nchi ya Zanzibar, alisema matarajio yake makubwa katika uchaguzi ujao ni kwamba utafanyika katika mazingira ya amani na utulivu.
Alisema ni matumaini yake kwamba mara hii ataongoza na kuibuka kuwa rais endapo uchaguzi utakuwa huru na haki. “Kama wananchi wa Zanzibar watanipigia kura kwa wingi nawahakikishia hakuna mtu yeyote atakayechezea ushindi wangu,” alisema Maalim Seif. Akizungumzia afya yake kuelekea Uchaguzi Mkuu, Maalim Seif alisema anagombea nafasi hiyo akiwa mzima wa afya na hana shaka, hivyo wananchi waondoe hofu katika hilo. “Nachukua fomu ya urais na matarajio yangu makubwa ni kushinda katika uchaguzi mkuu ambao utafanyika katika mazingira ya amani,” alisema.
Kuhusu masuala ya uchumi, alisema atahakikisha ajira zaidi kwa vijana zinaimarishwa na kuongeza maeneo huru ya uchumi. “Hivyo ndivyo vipaumbele vyangu nikichaguliwa na wananchi wa nchi yetu ya Zanzibar kuwa Rais katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa,” alisema. Hafla ya Maalim Seif kuchukua fomu ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwamo mawaziri katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa kutoka CUF. Maalim Seif aliwataka wanachama wengine kujitokeza kugombea nafasi hiyo kwa kuwa ni haki yao kikatiba.

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO

No comments:

Post a Comment