Thursday, May 14, 2015

WAZANZIBARIIIII HAAAAAA AHAAAAAA HAMAD RASHID ANALETWA NA MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA AJE AWAKOROGE AKILI MSAHAU MAMLAKA KAMILI WAZANZIBARI SOTE TUSEME HATUMTAKI SHEIN WALA HAMAD RASHID


MWAKA HUU NI KUM DELETE HAMAD RASHID NA KUMFUTA KABISA AKISALIMIYANA NA FIRAUNI MDOGO NCHINI TANGANYIKA

Unapokuwa mfwatiliaji sana wa siasa za nchi ya Tanganyika wakoloni weusi / Zanzibar nchi ya amani , unaweza kupatwa na kichaa!!
tunaporudi nyuma kidogo katika harakati za siasa zilizopita nchini Zanzibar tutakumbuka hadithi za dada yetu Naila Jidawy!! alipojitia katika siasa za CUF na kujifanya mshabiik mpaka kuweza kuchaguliwa kuwa mbunge wa kuteuliwa kwa chama hiki cha CUF. tukawa nae mstari wa mbele katika kupigania haki na kusimama kwenye viriri vya majukwaa kuipinga CCM na serikali zake. Muda haukuwa mrefu dada yetu huyu aliteleza kisiasa na kufukuzwa katika chama kwa sababu ambazo mpaka hii leo hazikuelezwa wazi, huwenda zilisitiriwa au vyenginevyo.
CUF waliamini kuwa baada ya kutekeleza khatuwa hio ya kumfukuza angesitishwa ubunge wake bungeni Giningi Dodoma, na baada yake wangeweza kumchaguwa mbunge mwengine kuziba mahala pake, haya hayakuwezekana. na sababu kuu ni mwenyewe Naila Jidawy kwenda kujitetea mahakamani asalie bungeni mpaka ngwee yake imalizike. na kwa msaada wa CCM na Mahakama bandia maana tunaona wanavyo wafanya Masheikh wetu basi dada yetu Naila Jidawy akawa mwenye bahati nzuri mahakama ikambeba na ameweza kuendelea na ubunge wake mpaka mwisho ni nchi hizi mbili tu mambo haya.
Mambo kama haya yamejirudia tena kwa Hamad Rashid. baada ya kufukuzwa chama kwa sababu zisizojulikana wazi mpaka hii leo, mahakama iliweza pia kumhifadhi aendelee na ubunge wake mpaka hivi sasa au hii leo kwa kujuwa kuwa bunge linamalizika muda wake na kusimama mbele ya bunge na kutamka hadharani yakuwa analihama bunge kwa mwaka huu na anatangaza hadharani kuwa ana nia ya kupigania uraisi kwa mwaka huu wa nchi ya Zanzibar, kama alivyofanya Naila Jidawy huko nyuma. haya mawili yanafanana sawa sawa!!
Naila Jidawy kwa wakati ule alitumiwa na system ya CCM na kushajiishwa apiganie uraisi kwa njia ya NCCR ili iwezekane kuzipunguza kura za CUF na kuisaidia CCM. Na bila ya shaka yoyote alikuwa ameahidiwa jambo ambalo mpaka hii leo imekuwa siri!! lakini kwa kuwa hakuweza kutekeleza kazi ile aliopewa kwa kuwa mahakama alithibitisha kuwa bado ni mwanachama wa CUF hakukuwezekana kuifanya kazi ile na alikataliwa kuingia katika kinyanganyiro cha uraisi. Na ikawa ndio mwisho wa hadithi ile. Na CCM ilimtupilia mbali kwakuwa hawakupata maslaha yao kwake. na juu ya yote yale baadae CCM na Serekali lake walianza kumuandama kwa kumvunjia biashara zake paje za utalii,ili asipate hata kula yake na sina shaka mpaka hii leo hakusimama imara na mambo yake kwa jinamizi hili la CCM kumtimba.
Leo hii Hamad Rashid anapitishwa njia ileile ambayo Naila Jidawy alimokanyaga!! hapana shaka yoyote kwakuwa Hamad Rashid ameshafilisika kisiasa, anatafuta pa kuchupia!! na kwakuwa serikali za sasa za Zanzibar ni za shirikisho za vyama viwili hakuna shaka kuwa ametumwa aingie ulingoni kuisaidia CCM ishinde kwa kuzigawa na kuzipunguza kura za CUF pemba na Unguja ili kuisaidia CCM ishinde ili aweze kugaiwa angalau fupa la kungongona hapo itakaposhinda CCM mwaka huu ikiwa itashinda kwa wizi na wananchi wakamuwa kulala!! anasahau kama alietoka CUF ni yeye peke yake. na hana wafuwasi wowote huko wawi alikosimamia uchaguzi na kuupata uongozi wa bunge kwa jimbo hilo. sasa kwa mtizamo wangu huu ndio mwisho wa safari yake ya kisiasa!! wengi watu wa aina hii wametoweka!! fatma majimbi, na wenzake wako wapi hii leo...? Msabaha, na wengine chungu nzima wako wapi....? Tusimsahau Mapalala yuko wapi...?  Marhem Omar Awesu Dadi (Mwenye enzi Mungu amlaze mahala pema peponi) na wengine  kuna kina Gosej na wengine na wengine, chama cha CUF kipo pale pale hapana hapana hapana chezeyaaaa.
Sasa yaliobaki tungojee ili tuone mwisho wa safari ya huyu kibaraka mpya ambae amekivaa kibwebwe kuipinga CUF, chama ambacho ndio kiliomlea !!

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

No comments:

Post a Comment