Saturday, July 11, 2015

MAFISADI WA EPA NA ESCROW WAUWANA WA KICHINJANA WENGI WAO WAFA KIHORO GININGI DODOMA

Lowassa+Kukatwa+Photo+Cartoon+Front
KAZI KWENU SISI TUKO PALE PALE ZANZIBAR YENYE MAMLAKA KAMILI

Nchini Tanganyika kuna killa dalili ya kusambaratika kwa chama cha CCM mafisadi wakubwa mwaka huu kuelekea katika uchaguzi mkuu wa october 2015. kumedhihirika ndani ya chama hiki kikongwe kilicho zeka kabisa kihoi bin tabani kuwa kuna mipasuko ya ndani kwa ndani, ambayo inafukuta na kusababisha wanachama pamoja na viongozi wao kutokusikizana na kutafautiana msimamo yao kwa kuwa kila moja anafikiria tumbo lake na wapambe wake watakula vipi.
Bila ya kusahau kule kulewa na madaraka na kusababisha ufisadi wa kupindukia wa kufuja rasilmali za nchi na kusababisha wengi wa viongozi wao kuhusishwa na ufisadi huo na kuanikwa ndani ya bunge hadharani, na hakuna khatuwa yoyote ambayo imechukuliwa kuwarudi wahalifu hao walio ibaa mamillioni kwa mamillioni, kinyume chake ndio hao hao ambao hawana hata haya wala hawajuwi vibaya hii leo wanaupigania uraisi kwa hali na mali na kutumia yale yale mamillioni walio ibaa kutafuta uraisi na kwa njia ile ile ya mirungura na rushwa kwa kukosa haya na wala kuona vibaya, kwa kuamini yakuwa Watanganyika bado watawachaguwa na kuendelea kugawa keki ile ile milele au pia kufikiri kuwa Watanganyika bado wamellala haaaa !!
kwa mtizamo wa haraka haraka kuna killa dalili baada CCM mafisadi kujidai kuwatowa mafisadi na kujidai kubakisha wanao waona wao kuwa sio mafisadi lakini wanachi wanajuwa kuwa CCM nzima ni mafisadi hata hao walio bakia pia ni mafisadi, kuna kila dalili ambayo inaonyesha kuwa yoyote atakaechaguliwa kubeba bendera ya chama cha CCM mafisadi atabwagwa chini chali nyanga nyaga, ndembe, ndembe, mlalo wa chali, kifo cha mendee!!! Hali inavyokwenda na kuendelea hivi sasa si nzuri kwa upande wa watawala na chama chao CCM mafisadi Tanganyika na hata hao walio toka Zanzibar kwenda kubebeleza tonge huko Giningi Dodoma. na kila siku zikiendelea mambo yana zidi kuwaharibikia zaidi na zaidi. haya yanatokana na ulewaji wa madaraka wa chama cha CCM mafisadi kwa kuamini ya kwamba siku zote wataendelea kutawala. na wao tu ndio wenye uwezo na haki ya kuitawala Tanganyika nzima na hata nchini  Zanzibar pia. kinyume na hilo haiwezekani.
Wanasahau kusoma nyakati, yakuwa ule wakati ambao CCM mafisadi ilikuwa ikingara hivi sasa umepitwa na wakati. Watanganyika wameshaichoka CCM mafisadi na huko Zanzibar ndio kabisa hawataki hata kukiona au kukisikia chama cha CCM mafisadi nani ya nchi yao ya Zanzibar, na hili limetokana na chama chenyewe kulewa madaraka hata kufikia kudharau hata sheria zao mama ndani ya chama chao wenyewe ambazo wamezitunga wenyewe na kushindwa kuziheshimu au kuzibadilisha ili tu mambo yao yawaende wanavyotaka wao na ufisadi wao. Imefika sasa wakati wa chama hiki kuondoka madarakani wakitaka wasitake. Hivi sasa chama hiki kimefikia wakati hakina masikizano wenyewe kwa wenyewe, na kila wakiendelea na haya watakaonufaika khasa ni Wananchi kwa mara ya kwanza kabisa katika maisha yao, ambao wamejidhatiti mwaka huu kwa kusahau khitilafu zao na kuungana kwa jina moja la UKAWA na kudhamiria kukingowa chama cha mapinduzi madarakani mwaka huu !! na hali ya chama cha CCM kilivyofikia kwa hivi sasa , kuna killa dalili ya kuangushwa na UKAWA katika uchaguzi wa mwaka huu Tanganyika na Zanzibar pia, haya yako wazi tuwe Wananchi wamechoka na ufisadi na wamechoka na hawa mafisadi wamechoshwa na vitimbi na uwongo wa hawa mafisadi CCM mafisadi bye bye........
KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

No comments:

Post a Comment