Tuesday, July 7, 2015

NEC; HAWANA UWEZO WAKUTAMBUWA WAPIGA KURA HARAMU ZANZIBAR TUNAWATAMBUWA NA TUKIWAFICHUWA MBONA MNATUPIGA RISASI....???


Hakuna njia maalum ya kuthibitisha uraia wa watu katika usajili unaoendelea wa wapiga kura kwa njia ya electroniki, Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC) imekiri huko nchini Tanganyika. NEC pia imesema kwamba ni jukumu la wananchi wa maeneo hayo kuwatambua na kuwazuia watuhumiwa wa usajili haramu. Katika mahojiano maalum na wandishi jana jijini Dar es Salaam nchini Tanganyika na (NEC) Mkurugenzi wa Uchaguzi, Julius Malaba alikiri kwamba; “Hatuna utaratibu wa kutambua uraia wa mtu kabla ya kujiandikisha” NEC inakusudia kuweka hadharani kuonyesha majina ya wapiga kura waliosajiliwa ili kuruhusu wakazi wa eneo Fulani kuyawekea vikwazo majina wanayoyatilia shaka,(( mbona Zanzibar tukizui mamluki wenu munao waleta kupiga kura mnatupiga risasi Wakoloni nyie Weusi Tanganyika.)) na kwamba watu hao wataitwa ili kuthibitisha utambulisho wao pamoja na ukaazi,” alifafanua. “Umma utambue, usajili sio mwisho wa mchakato, Majina yote yatapitiwa kuthibitishwa na mawakala husika katika maeneo yao,” alisema watu amabao wanatiliwa shaka watahojiwa, watatakiwa kuleta nyaraka kuthibitisha uraia na ukaazi wao.((huku Zanzibar musha wapa ZAN ID ili tusiwatambuwe ila tunajuwa sisi vya kuwauliza wakiweza kujibu sawa wakishindwa tunajuwa ni mamluki wenu))
Hayo yakitokea wiki iliyopita ,imethibitishwa zaidi ya wageni 12,000 wameandikishwa katika usajili wa wapiga kura ( BVR) katika wilaya moja tu ya Kyerwa na takwimu inaonesha kuna idadi kubwa zaidi katika wilyaya nyengine nchini. “Tunafahamu kwamba kuna wageni wamesajiliwa … ndio maana tumeamua kuthibitisha majina kabla ya kukamilisha zoezi,” aliendelea kusema. Ripoti hiyo ilithibitishwa na Katibu wa wilaya ya Kyerwa Josephat Kakuru, ambaye alisema wahamiaji haramu wengi wameingia kutoka nchi jirani za Uganda, Rwanda na Burundi.(( kama nyinyi Watanganyika munavyo ingia Zanzibar kwa njia ya CCM)) Kakuru, alisema wahamiaji haramu waliosajiliwa kiasi cha 8000 wamepokonywa vitambulisho vyao na kufutwa usajili wao. ((sasa mbona na sisi Zanzibar tukiwapokonya watanganyika vitambulisho vya ZAN ID Vuai analalamika...?)) “Polisi na vyombo vingine bado wanaendelea na kazi juu ya suala hili ,ili kuhakikisha kuwa kadi zote walizopewa wahamiaji haramu zinapatikana na kuchukuliwa hatua inayostahili.((Zanzibar polisi wanashirikiana na waficha nyuso wahuni wa Shein na Haji Omar Kheri kuwapiga risasi wazanzibar wanao zui hao mamluki wenu)) “Wale wote waliohusika katika kashfa hiyo watakamatwa na kupelekwa mahakamani kujibu mashtaka yao,”((Zanzibar wanalindwa na kupelekwa na mabasi na kupewa pahali pazuri paa kulala na kula na kuhaidiwa uchaguzi ukimalizika watapatiwa kazi na nyumba za kuishi)) aliongeza akitoa mfano kwamba hata kama awe ni kiongozi yeyote wa serikali za mitaa ambao atasaidia wahamiaji hao haramu.((Haji Omar Kheri,Shein anajuwa kaufyata,Balozi mkazi,kambi ya jeshi ndizo zinazo tumiwa kujiandikisha na kuhifadhiwa hapa Zanzibar))
Katika hatua kama hiyo, wiki iliyopita watu wanne, ikiwa ni pamoja na Wakenya watatu, walikamatwa na polisi kwa ajili ya kuingia Tanganyika kinyume cha sheria na kusajili mara mbili katika BVR.((Zanzibar kuna Watanganyika,Wakenya,Warundi,Wanyaruwanda na Wakongo wote wamejiandikisha na BVR na wanalindwa na polisi na jeshi na waficha nyuso wahuni)) Kwa mujibu wa afisa uhamiaji Wilayani Bunda , Elizeus Mushongi, Wakenya hao walikamatwa kufuatia habari zilizotolewa na wasamaria wema.((Zanzibar wasamaria wema wanapigwa risasi au jela)) Taarifa fupi kutoka wilaya ya Bunda ilisema ,Wakenya hao walikuwa wamejiandikisha katika vituo zaidi ya viwili,wameshakamatwa na watafikishwa mahakamani mara moja uchunguzi utakapokamilika.((Zanzibar tuna ushahidi wa pic na video na hawakamatwi wanalindwa)) Katika hatua nyingine Mwandishi Renatus Masuguliko anaarifu kuwa, kiasi cha watu watano, ikiwa ni pamoja na mwalimu mmoja wamekamatwa na polisi katika Wilaya ya Nyang’hwale , Mkoa wa Geita kufuatia wizi wa mashine ya kujiandikisha wapiga kura.(( hiyo mashine basi labda ndio wanayo tumia hao CCM kuandikisha mamluki wao hapa Zanzibar)) Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale Ibrahim Marwa alisema tukio lilitokea mwishoni mwa wiki katika shule ya msingi ndani ambapo mashine ilikuwa imehifadhiwa na kwamba uchunguzi unaendelea. Polisi wamethibitisha tukio hilo na kazi ya kuipata mashine((iko Zanzibar njoni muje muichukuwe)) hiyo bado inaendelea,kwa mujibu wa polisi,mahali ilipokuwa mashine hiyo ,hakuna dalili zozote za Mlango kuharibiwa.
KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

No comments:

Post a Comment