Monday, September 14, 2015

VIDEO-NCHINI ZANZIBAR CCM WAMEZINDUWA RASMI KAMPENI SHEIN AAHIDI KUDUMISHA MAPINDUZI. HAHAHAHA


G-Solo "muda wa vitendo"



Chama cha Mapinduzi (CCM) nchini Zanzibar leo wamezindua rasmi kampeni za kitaifa kuelekea uchaguzi mkuu mwezi Oktoba mwaka huu. Shughuli hizo za uzinduzi zimefanyika kwenye Uwanja wa Kibandamaiti visiwani humo na CCM nchini Zanzibar wazindua rasmi kampeni,  kuhudhuriwa na viongozi wa juu wa chama hicho akiwemo Rais Jakaya Kikwete raisi wa nchi ya Tanganyika, Rais mstaafu wa nchi ya Tanganyika Benjamin Mkapa na rais wa awamu ya pili wa nchi ya Tanganyika, Ali Hassan Mwinyi.
Kwa awamu nyingine, Shein amepewa ridhaa ya kupeperusha bendera ya CCM kwa ngazi ya urais akipambana na wagombea wengine wa upinzania akiwemo Maalim Seif Sharif Hamad wa CUF anayeungwa mkono na Ukawa na wananchi wengi kwa ujumla.
 Shein amesema ataendelea kuyalinda, kuyatetea na kuyaendeleza mapinduzi yaliofanywa nchini Zanzibar 1964 kwa manufaa ya watu wake. Pia amesisitiza kuwa umoja, amani na utulivu ndiyo nguzo ya maendeleo ya taifa lolote duniani, hivyo serikali yake itahakikisha nchi ya Zanzibar inaendelea kuwa na umoja, amani na utulivu.
Kama ilivyo kwa nchi ya Tanganyika, wazungumzaji takriban wote waliopewa nafasi ya kuzungumza walitumia muda mwingi kuuzungumzia upinzani hususani wagombea wa Ukawa akiwemo Maalim Seif na Juma Duni Haji badala ya kuzungumza nini watawafanyia wananchi na vipi watawatatulia matatiyo yao yanayo wakabili kila siku kama maji safi,umeme,kuwa na uhakika wa milo mitatu waitay wao si kula mlo moja wa kubahatisha,hospitali ziwe na huduma nzuri na dawa,skuli za kisasa sio mabanda ya kufugia kuku hawakusema lolote wao walikuwa bizi kushambulia upinzani.
Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM taifa, amemkabidhi Dk Shein Ilani na Katiba ya chama hicho kama nyenzo muhimu anazopaswa kuzitumia wakati wote wa kampeni ili kujipatia ushindi Oktoba 25. Mkutano huo kama ilivyo mikutano mingine ya kisiasa, umehudhuriwa na idadi kubwa ya wananchi waliofika kusikiliza sera za CCM kwa bahati mbaya hawakuzisikia.KILA MZANZIBARI ATAKAE IPIGIA KURA CCM ILI IBAKI MADARAKANI AJUWE NA YEYE ANACHANGIA KUFUNGWA KWA MASHEIKH NA KUTHALILISHWA KWAO NA KUENDELEZA DHULMA KATIKA NCHI YA ZANZIBAR UKAE UKIJUWA UTAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA,KUDHULUMIWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

No comments:

Post a Comment