Thursday, September 17, 2015

POMBE MAGUFULI KATIKA JIMBO KASHINDWA KUWANUNULIA WALIMU CHAKI ZAKUANDIKIA WANAFUNZI NA KUWAVUTIA MAJI NA WANA ZIWA JIMBO TU ATAWEZA KUWAPA WANANCHI WA NCHI NZIMA....??? SIANGELIFANYA CHATO KWANZA

Mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika Uwanja wa Standi ya zamani, Chato, mkoani Geita jana

Wakati mgombea urais wa Chadema chini ya mwamvuli wa Ukawa, Edward Lowassa akiiteka Wilaya ya Chato ambako ni nyumbani kwa mgombea urais wa CCM, Dk John Magufuli kwa kufanya mkutano mkubwa wa kampeni, Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wilayani humo, Lucas Michael alitumia nafasi hiyo kueleza kilio cha walimu nchini na kumponda Dk Magufuli kwa kushindwa kutetea maslahi yao.
Lucas ambaye baadaye alilieleza Muandishi wetu kuwa hawezi kujuta kwa kutoa kauli hiyo hadharani akieleza “sijafanya kosa nimesema ukweli”, akiwa jukwaani alisema Dk Magufuli ambaye alikuwa mbunge wa Chato amewatupa walimu wa wilaya hiyo kwa madai kuwa wananunua wenyewe chaki, hawalipwi fedha za safari baada ya kustaafu na Halmashauri ya wilaya hiyo inagoma kuwasomesha.
Wakati mwalimu Michael akieleza hayo, Lowassa akizungumza katika mkutano huo uliofanyika katika stendi ya mabasi ya zamani mjini Chato na kuhudhuriwa na maelfu ya wananchi waliomsubiri kuanzia saa nne asubuhi hadi saa 10 jioni, aliahidi kufufua viwanda vilivyopo mkoani humo na kuvuta maji kutoka Ziwa Victoria baada ya kuelezwa kero za wananchi wa wilaya hiyo na mgombea ubunge, Benedicto Lukanima (Chadema).
Michael aliyekuwa ameshika kipeperushi chenye picha ya Lowassa alimuomba kada mpya wa Chadema, Tambwe Hiza aliyekuwa akizungumza jukwaani kabla ya Lowassa kufika eneo hilo, kuwa ana ujumbe mzito kwa walimu wa Chato.
“Nimelazimika kuja hapa kuyasema yafuatayo. Tanu ilipata nguvu baada ya Mwalimu Julius Nyerere, Oscar Kambona na wafanyakazi wengine kuungana na Rashid Kawawa kudai uhuru wa Tanganyika. Bila wafanyakazi kujitetea na kudai haki yao hakuna maisha ya kweli na ya uhakika.
“Namuuliza Dk Magufuli mbona katika halmashauri yake haisomeshi wafanyakazi, mbona wakistaafu hawapewi fedha za safari kulejea makwao, mbona walimu tunachanga fedha kununua chaki,” alisema na kushangiliwa na wananchi.
Huku akirejea kauli ya Dk Magufuli aliyotoa hivi karibuni kwamba wananchi wamchague kwa kuiga mfano wa alichokifanya Chato Michael alisema, “Wanasema tuchague CCM kwa kuiga Chato sasa tunachagua nini kwa haya yanayotokea Chato.”
“Kazi ya mwalimu ni kufundisha elimu ya darasani na ya watu wazima. Walimu wasiwe waoga wawafundishe ukweli watu wao. Bendera ya taifa ina rangi ya njano, kijani, nyeusi na bluu huku nyeupe ikiwa imeizunguka bendera hiyo hivyo walimu wafanye uamuzi sahihi wakati sahihi na wakati ndiyo huu,” alisema Michael na kuibua shangwe katika mkutano huo.
Michael alilieleza Muandishi wetu kuwa ni mwalimu wa Shule ya Sekondari Chato tangu mwaka 2007 na kwamba alianza kazi ya ualimu mwaka 1987.
“Nimekuwa mwenyekiti wa CWT hapa Chato tangu Machi mwaka huu. Sihofii kufukuzwa kazi kwa sababu sijavunja sheria. Jambo linaloniuma zaidi ni kitendo cha walimu wanaoonekana kuunga mkono vyama vya upinzani kuadhibiwa na wale wanaounga mkono CCM kuachwa. Jambo hili si sahihi kabisa,” alisema.
KILA MZANZIBARI ATAKAE IPIGIA KURA CCM ILI IBAKI MADARAKANI AJUWE NA YEYE ANACHANGIA KUFUNGWA KWA MASHEIKH NA KUTHALILISHWA KWAO NA KUENDELEZA DHULMA KATIKA NCHI YA ZANZIBAR UKAE UKIJUWA UTAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA,KUDHULUMIWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

No comments:

Post a Comment