Friday, June 24, 2016

VIDEO-UCHAGUZI ZANZIBAR HAUJAKWISHA NA MSHINDI HAJATAGAZWA NDIO MAANA MNATUPIGA RISASI NA KUTUIBIA NGOMBE WETU

Rais John Magufuli akiongea na Dk Shein katika hafla ya sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar
RAIS Pombe Magufuli amepuuza maalamiko ya Wazanzibari kwamba, Chama Cha Mapinduzi (CCM) licha ya kukataliwa, kimelazimisha kurudi madarakani kwa kutumia jeshi lao la Makaburu Weusi Tanganyika na Kumuweka Tena Shein japo kuwa wamekataliwa  na amempongeza Jecha Salim Jecha, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (ZEC), kwa kile alichosema “ametimiza wajibu wake wa kusimamia uchaguzi mkuu wa Zanzibar wa mwaka jana vizuri.” haya Wazanzibari mlio kuwa mkijidanyanya kuwa Pombe Magufuli ni Rais Mzuri atasimamia Haki huyo hapo anaipogeza  HARAMU Mpoo Wazenji....??

Kwa kauli hiyo ambayo Pombe Magufuli ameitoa leo kwenye hafla ya kukabidhiwa ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa Tanganyika (Tanzania) Zanzibar uliofanyika mwaka jana, hajabadilisha msimamo kuhusu mgogoro wa kisiasa wa nchi ya Zanzibar uliotokana na uchaguzi huo hii nikuonyesha na kuwajulisha Wazanzibari kuwa yote yanayotokea Zanzibar yana Baaraka Zake.
Rais Pombe Magufuli amesema, uamuzi alioufanya wa kupeleka Zanzibar askari wengi wa vikosi vya ulinzi na usalama kulinda ili uchaguzi wa marudio wa 20 Machi 2016 uwe wa amani na salama ulikuwa sahihi na kwamba, naye alitimiza jukumu lake kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa (Tanzania.) Mnasikia maneno hayo.
Amesema, hakuna uchaguzi unaokosa kasoro hata ndogo lakini anashangaa kwamba, wapo watu wanahangaika mpaka nje ya nchi kuieleza vibaya serikali kwa kuwa, nilisema siwezi kuingilia tume ambayo ni huru.“Ni kweli sina mamlaka ya kuingia Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ambayo ikifanya uamuzi haiwezi kuhojiwa lakini nilipochukua hatua za kuimarisha ulinzi, nilitimiza wajibu wangu,” amesema.
Hata hivyo amesema kwa kurudia kuwa, uchaguzi umwekwisha nchini na sasa ni wakati wa kuwatumikia wananchi katika maendeleo.“Walewale waliokuja kunitaka niingilie maamuzi ya tume nikakataa wamekuwa wanaisema serikali ninayoongoza,” amesema bila kutajia jina la mtu huyo lakini alikuwa akimlenga Maalim Seif Sharif Hamada, Katibu Mkuu wa CUF.
Maalim Seif yupo ziarani nchini Marekani, Canada ambapo amekuwa akieleza hali halisi ya uchaguzi wa nchi ya Zanzibar namna ulivyovurugwa na Serikali ya CCM kwa lengo la kuendelea kubaki madarakani kwa guvu za mtutu na majeshi.CUF chini ya Maalim Seif ambayo ndio chaguo la watu kuwa ndiye rais wa Zanzibar aliyechaguliwa kihalali na wananchi, kinapinga uamuzi wa Jecha kufuta uchaguzi uliofanyika Zanzibar tarehe 25 Oktoba 2015 kwa kuwa, hakuwa na mamlaka ya kisheria ya kufanya hivyo.
Jecha alifuta uchaguzi huo tarehe 28 Oktoba 2015 kwa madai uliharibika na kisha kusimamia ualioitwa uchaguzi wa marudio wa tarehe 20 Machi 2016.
Baada ya uchaguzi huo Jecha alimtangaza Dk. Shein, mgombea wa CCM kuwa mshindi wa urais.
UCHAGUZI HAUJAKWISHA ZANZIBAR NA MSHINDI HAJATANGAZWA MNAJIBARAUSHA NA KUJIPUMBAZA NA KULAZIMISHA WAZANZIBARI WAKUBALI HARAMU ZENU NA MUENDELEZO WAKUWAPIGA RISASI NA KUWAIBIA MALI ZAO HAMTA FANIKIWA NA MTADHALILIKA NA KUIBIKA HIZI NI BAADHI YA PICHA ZA WAZANZIBARI WALIOPINGWA RISASI NA VIKOSI NA KUIBIWA NGOMBE WAO NA VIKOSI HIVYO HUKO TOMONDO BADALA YA KULINDA MALI ZA RAI WANAIBA MALI ZA RAI.

No comments:

Post a Comment