Tuesday, August 30, 2016

JULIUS MTATIRO NIMEUPOKEA UTEUZI

Afbeeldingsresultaat voor julius mtatiro
NIMEUPOKEA UTEUZI…..
Ndugu zangu, nimepokea majukumu niliyokabidhiwa na Baraza Kuu la chama changu. Siwezi kuepuka majukumu haya muhimu kwa wakati huu ambapo chama kinahitaji mchango wangu. Niko IMARA sana, natambua nimepewa majukumu wakati gani na nianze na mguu upi kwenda mbele.
Uongozi ni MZIGO na si kazi nyepesi, nahitaji kusaidiwa, kushauriwa, kuombewa na kuungwa mkono na watu wenye nia njema na siasa za mabadiliko ya kweli hapa nchini, walio ndani na nje ya CUF.
Natambua kuwa wapo wana CUF wenye sifa, uwezo, vigezo na busara kunishinda, lakini kwa sasa chama kimeona naweza kuuungana na wenzangu kukisimamia. Naahidi kuwa ntatoa uongozi wa KISASA wenye kushughulikia MASUALA. Ntatimiza wajibu wangu bila hofu yoyote kama kawaida yangu na ntatoa UONGOZI WA PAMOJA (Collective Leadership) kwa kila mwenye nia safi na CUF na mabadiliko.
Nitakuwa mhimili imara katika kipindi hiki cha mpito, kuhakikisha CUF inafanya kazi zake na inaimarika ili kujenga uwezo wa ndani, kulinda mtandao wake na kujitanua katika maeneo yote ya Bara na Zanzibar – lakini pia, ntahakikisha ushirikiano wa CUF na vyama vyote vyenye nia njema ya kupigania mabadiliko hapa Tanzania, unazidi kuimarika ili mwisho wa siku watanzania wafaidike na juhudi za mabadiliko hayo.
Mtanzania yeyote anaweza kuwasiliana nami moja kwa moja kwa njia za ujumbe mfupi na WHATSUP kwa namba +255787536759, na Barua Pepe: juliusmtatiro@yahoo.com, 
na atajibiwa. Tutaendelea kuwa karibu kwa hali na mali.Nakishukuru chama changu kwa kuniamini. Nawashukuru wanachama wote na watanzania wenzangu walionitumia salamu za pongezi ambazo sina uwezo wa kuzijibu zote.
Mungu awabariki sana.
Julius Mtatiro,
Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi,
The Civic United Front (CUF),
29 Agosti 2016.

VIDEO-PROF LIPUMBA SIASA SI BONGO FLAVA KUWA UTOKE VIPI AU UTAFUTE KIKI

LIPUMBA TOKEJE MMM MWENZENU TOKEJE CCM WAMENIPIGA NA CHINI
NA CUF SIPENDWI TENA LIPUMBA TOKEJE MMM MWENZENU TOKEJE
Sijui Chiziiiii Profesor Mzima anababaika mara natoka mara nataka .Njaa tu inamsumbua maskini unajua mtu ukiwa huna Imani ya Kidini ktk wakati huu tulionao basi ni shida sana .Profeaso Kuna nchi zinakutaka nenda ukawasaidie ktk kuburesha uchumiii wao sasa unangangania kitu gani hebu wacha bwanaa, Kidhabizabina huko huku wala huku kila chenye mwanzo huwa na mwisho hebu elewa hivyoooooo.Weye mnyamwezi gani usiekuwa na msimamoooo.Halafu tena eti ni Msomi sasa hii PROFERSOR si jui si ya kweliiiiiii. Inanitia wasi wasi.

Monday, August 29, 2016

VIDEO-UDIKTETA UCHWARA NCHINI TANGANYIKA UNAENDELEA VIONGOZO WA KUU WA CHADEMA WAKAMATWA

MWANA SHERIA AWADHI ALI SAIDI HAKI YA VYAMA VYA SIASA KUFANYA
MAANDAMANO NA MIKUTANO YA HADHARA
Viongozi wa Chadema wamekamatwa na polisi na kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar es Salaam nchini Tanganyika kwa ajili ya mahojiano.

Akizungumzia kukamatwa kwa viongozi hao Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alisema; “Tulikuwa kwenye kikao cha Kamati Kuu kilichojumuisha wajumbe na wabunge kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya chama. Jumla ya wajumbe walikuwa 170. Tukiwa kwenye kikao walikuja watu wanasema tunatakiwa polisi kwa sababu tumekiuka agizo lililokataza mikutano.”

Waliotakiwa kufika makao makuu ya polisi, ni pamoja na mwenyekiti wa chama hicho taifa, Freeman Mbowe; mjumbe wa Kamati Kuu na waziri mkuu mstaafu, Edward Lowassa; Katibu Mkuu, Vicenti Mashinji na naibu katibu mkuu (Bara), John Mnyika.

Mkutano wa kamati kuu ya Chadema, umeitishwa ili kujadili ufanikishaji wa maandamano ya oparesheni UKUTA.

VIDEO-CUF: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Afbeeldingsresultaat voor Nassor Ahmed Mazrui
WALIKUWA CUF WAKAPANDA WAKALISHWA PESA UCHWARA
WAIUWE CUF SASA WANASHUKA KWA KASI NA KUTETEMEKA

Ndugu Waandishi wa habari,
Awali ya yote naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia uhai na uzima wa afya na tukaweza kukutana hapa asubuhi hii ya leo. Tunamshukuru Mwenyezi Mungu pia kwa kuijaalia nchi yetu kuendelea kubaki katika hali ya amani na utulivu licha ya matatizo mengi yanayotukabili.
Pili, nichukue fursa hii kukushukuruni nyinyi waandishi wa habari kwa kuitikia wito wetu na kuja kutusikiliza. Ni imani yangu kuwa kama ambavyo mmekuwa mkitupa mashirikiano mazuri katika kuwafikishia wananchi yale ambayo chama chetu kupitia kwenu kimekuwa kikiyatolea taarifa, kwa uzito wa kipekee taarifa hii nayo mtawafikishia Watanzania wote kupitia vyombo vyenu vya habari.
Ndugu Waandishi wa habari,
Tumewaita leo hii kuwaeleza juu ya maazimio ya kikao cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa katika kikao chake cha dharua kilichofanyika jana, Jumapili ya tarehe 28/08/2016 Katika ukumbi wa Makao Makuu ya Chama, ofisi za Vuga. Kikao hicho kilichoongozwa na Mwenyekiti wa muda Mhe, Hamidu Hassan Bobali, Mbunge wa Jimbo la Mchinga kilihudhuriwa wa Wajumbe 46 katika ya Wajumbe 60.
Ndugu Wandishi wa Habari,
Kama mnavyojua tarehe 21/08/2016 Chama Cha Wananchi – CUF kilikuwa na Mkutano Mkuu Maalum wa Taifa uliofanyika katika ukumbi wa Blue Pearl, Ubungo Plaza, Dar es Salaam. Mkutano huo ulikuwa na agenda mbili kuu, ambazo ni:-
1. Kupokea barua ya Profesa Ibrahim Haruna Lipumba ya kujiuzulu nafasi yake ya uenyekiti ya tarehe 05/08/2015; na
2. Kufanya Uchaguzi wa kujaza nafasi zilizo wazi – Mwenyekiti Taifa, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wanne wa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa.
Kufuatia hujuma za makusudi zilizoandaliwa kwa mashirikiano ya maadui wa ndani na nje ya chama, aliyekuwa Mwenyekiti wa muda wa Mkutano Mkuu Maalum, Mhe Julius Mtatiro alilazimika kuakhirisha Mkutano ule mara baada ya kumalizika kwa ajenda ya kwanza ambapo Mkutano Mkuu uliridhia kujiuzulu kwa Profesa Ibrahimu Haruna Lipumba kwa azimio lililoungwa mkono na wajumbe 476 dhidi ya wajumbe 14 waliokataa. Hivyo basi agenda namba 2 haikuwahi kukamilishwa, na kwa hivyo haikufanyiwa maamuzi.
Kikao cha Baraza Kuu la Uongozi, kilichokaa jana kimejadili kwa kina juu ya hujuma za kuvuruga Mkutano Mkuu Maalum wa tarehe 21/08/2016. Baraza kuu limesikitishwa sana na kitendo kile ambacho mbali ya kukisababishia chama hasara ya zaidi ya Shillingi milioni 600, pia kimepelekea kuharibu taswira ya chama ndani na nje ya nchi.
Baraza Kuu lilipata nafasi ya kupokea maelezo ya kina kutoka kwa wajumbe mbali mbali hasa wale wanaotokea Tanzania Bara walioeleza kwamba hujuma zilizofanywa kuvuruga Mkutano Mkuu Maalum wa Taifa wa tarehe 21 Agosti, 2016 hazikuwa za bahati mbaya au za kushtukiza bali ni matokeo ya njama na mbinu ovu na chafu ambazo zimekuwa zikipangwa na kutekelezwa chini kwa chini kwa muda mrefu. Wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa walieleza kwa ushahidi jinsi baadhi ya viongozi wa Chama walioaminiwa na kupewa nyadhifa za juu walivyogeuka na kuanza kutumiwa na maadui wa nje ya Chama kukihujumu Chama.
Baraza Kuu limezingatia kuwa CUF ni chama cha kistaarabu, ni Chama cha Kidemokrasia na ni Chama chenye kutoa matumini ya mabadiliko ya kweli kwa Watanzania walio wengi. Vurugu zilizojitokeza ni aibu na fedheha kwa chama chetu mbele ya macho ya Watanzania na wapenda demokrasia.
Baraza Kuu la Uongozi la Taifa limeridhika kwamba watu hao waliokuwa vinara wa vurugu na njama hizo ovu walipewa nafasi mara kadhaa kujirekebisha dhidi ya mwendo wao huo dhidi ya Chama lakini waliendelea na vurugu na hujuma zao hizo. Kwa hatua iliyofikia, Baraza Kuu limeona halina njia nyengine ya kukinusuru Chama isipokuwa kuchukua hatua kali na madhubuti kukilinda Chama ambao ni wajibu wake kikatiba.
Kwa msingi huu basi, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa kwa kauli moja (unanimously) limeamua kuchukua hatua za kinidhamu kwa viongozi na wanachama mbali mbali waliohusika kwa njia moja au nyengine katika kuchochea vurugu zile. Baraza kuu limechukua hatua mbili kubwa ambazo ni kutoa karipio kali, kusimamisha na kufukuza uanachama wahusika wote walioshiriki kuchochea vurugu hizo.
Viongozi waliopewa karipio kali kwa mujibu wa Katiba ya Chama, Ibara ya 83 (5)(b) ambao ni wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa ni:
1. Rukiya Kassim Ahmed na
2. Athumani Henku
Viongozi waliosimamishwa uanachama kwa mujibu wa Katiba ya Chama, Ibara ya 83 (5)(c), hadi hapo watakapopata fursa ya kujieleza mbele ya Baraza Kuu ni;
1. Prof Ibrahim Haruna Lipumba
2. Magdalena Sakaya
3. Abdul Kambaya
4. Ashura Mustafa
5. Omar Mhina Masoud
6. Thomas Malima
7. Kapasha M. Kapasha
8. Maftaha Nachumu
9.Mohamed Habib Mnyaa
10. Haroub Shamis
na
11. Mussa Haji Kombo
Mwanachama aliyefukuzwa chama ambaye alipata fursa ya kujieleza mbele ya Baraza Kuu na kikao kuamua kumfukuza chama kwa mujibu wa Katiba ya Chama, Ibara ya 83 (5)(c) ni aliyekuwa Kaimu Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Wazee wa CUF (JUWACUF), Shashu Lugeye.
Kufuatia maamuzi hayo, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa limewateua viongozi mbali mbali kukaimu nafasi mbali mbali zilizoachwa wazi.
Kwa kuzingatia kwamba kutokamilika kwa Mkutano Mkuu Maalum wa Taifa wa tarehe 21 Agosti, 2016 kulipelekea kushindwa kufanyika kwa uchaguzi wa Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Chama, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa limetumia uwezo liliopewa na Katiba ya Chama, Ibara ya 101 na 118, kuunda Kamati ya Uongozi ambayo itakuwa ikifanya kazi za Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti hadi hapo uchaguzi wa kujaza nafasi hizo utakapofanyika. Baraza Kuu la Uongozi limewateua wafuatao kuwa wajumbe wa Kamati hiyo ya Uongozi:
1. Mhe. Julius Mtatiro – Mwenyekiti;
2. Mhe. Katani Ahmed Katani – Mjumbe; na
3. Mhe. Severina Mwijage – Mjumbe.
Aidha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa, kwa kufuata Ibara ya 105 (1) na (3) ya Katiba ya Chama, limemteua Mhe. Joran Bashange kuwa Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Chama kwa upande wa Tanzania Bara na Mhe. Mbarala Maharagande kuwa Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma hadi hapo nafasi hizo zitakapojazwa rasmi kwa mujibu wa masharti ya Katiba ya Chama.
Mwisho, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa linawahakikishia wanachama na wapenzi wake na Watanzania wote kwa ujumla kuwa Chama Cha Wananchi – CUF kipo imara na makini na katu hakitoyumbishwa kwa hila na njama ovu na chafu zinazofanywa na maadui wa chama hichi. Tangu kuasisiwa kwake, CUF imeandamwa na maadui wa kila aina, na imepitia katika misuko suko mingi. Tunaamini hila na njama hizo ovu zimekuwa zikielekezwa CUF kwa kutambua kwamba Chama hichi ndicho kinachobeba dhamira ya dhati ya kuleta mabadiliko ya kweli hapa nchini.
Kutokana na umadhubuti, umakini na uimara wa Katiba ya Chama na safu ya viongozi wake, CUF imeweza kuvuka salama kila ilipoingia katika misuko suko hiyo na kwa hivyo, hata wimbi hili lililoonekana kukitikisa Chama limekabiliwa ipasavyo na sasa kazi iliyopo mbele yetu ni kuendeleza harakati za kisiasa za kuwaletea Watanzania wa Bara na Zanzibar mabadiliko wanayoyataka.
HAKI SAWA KWA WOTE
Nassor Ahmed Mazrui
NAIBU KATIBU MKUU CUF

VIDEO-NCHI HIZI KWA AHADI KALI KWA ZAIDI YA NUSU KARNE NA HAKUNA MOJA LIWALO-NCHI YA TANGANYIKA-NCHI YA ZANZIBAR

Afbeeldingsresultaat voor pombe magufuli na dr shein

Afbeeldingsresultaat voor pombe magufuli na dr shein

Afbeeldingsresultaat voor pombe magufuli na dr shein

Afbeeldingsresultaat voor dr shein apishwa 2016

Friday, August 19, 2016

VIDEO-FEDHEHA KWA BABUALI MKONO UMEKATALIWA HUKUTAKA KUONDOKA KWA HIYARI NA HISHIMA UTAONDOKA KWA KUFEDHEHEKA NA KUAIBIKA ASIYEKUBALI KUSHINDWA SI MSHINDANI SHEIN LIJUWE HILO

SIKILIZA HII NYIMBO LABDA ITAKUFUNZA KITU IKIWA UNA AKILI YA UWAZI
Dr Sheni awaambia washauri wake bora ningebaki Tanganyika kuwa Makamo wa Urais kuliko hichi kitanzi niliochotiwa cha kulinda Mapinduzi na aibu niliovikwa ya kuitwa kinganganizi cha madaraka na kulazimishwa kubaki madarakani. Awaambia Washauri wake akistaafu na yeye hatokaa Zanzibar bali atakimbilia bara kama Mzee Jumbe ,Mzee Abdul Wakil na Mzee Mwinyi kwani hata watoto wake wamechoka choko choko za Zanzibar za yeye kuitwa msaliti wa kuikoroga Zanzibar.Hadi kwenye MAzishi ya Mzee Jumbe mimi nimefanywa ndio kituko cha mitandao ya jamii inawaudhi watoto wangu. kama umechoka kweli siujuzulu tu kisha uwende zako huko Tanganyika kinacho kuzui nini kama si kinganganizi cha madaraka na kulazimisha kubaki madarakani ulikuwa ushashindwa uchaguzi ulikuwa ukubali tu basi haya yote yasingelikufika lakini ukajitia kungangania sasa unamlilia nani kama hukutaka kuondoka kwa heshima utaondoka kwa kudhalilika ndivyo ilivyo pia sasa hujachelewa bado jizulu tu.

Wednesday, August 17, 2016

VIDEO-MOUDLINE CASTICO ACHAKUTUTUKANA WAZANZIBARI KUMBUKA WEWE MWENYEWE SIO RAI WA NCHI YA ZANZIBAR UWAZIRI UMEUPATA KWA KUWEKWA NA MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA

Waziri%20Uwezeshaji,%20Wazee,%20Vijana,%20Wanawake%20na%20Watoto,%20Moudline%20Castico
Waziri aliyeletwa na Mkoloni Mweusi Tanganyika na kufanywa ati waziri wa uwezeshaji, wazee, vijana, wanawake na watoto, Moudline Castico nchini Zanzibar anza na haya matusi kututukana sisi na dada zetu CCM oyeee CCM oyeee
SERIKALI ya Haramu ya Shein na Gengi lake imekiri kuwa vijana wanaokwenda kufanyakazi nje ya nchi, wamekuwa wakikutana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia. (nyinyi wenyewe munawafanya nini siku za uchaguzi nyinyi si ndio wa mwanzo munao wadhalilisha kijinsi kisa hawajaipigia kura CCM leo mnasema nini nyinyi.)
Akizungumza na waandishi wa habari juu ya ati ‘Siku ya Vijana Duniani’,Waziri aliyeletwa na Mkoloni Mweusi Tanganyika na kufanywa ati Waziri Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto, Moudline Castico alisema Serikali ya Zanzibar imeshakaa na Ubalozi wa Oman na nchi zingine kuondoa matatizo yaliyojitokeza ya udhalilishaji. (mbona umeitaja Oman tu hizo nchi nyengine hukuzitaja au ndio mnaendelea na kasumba zenu za uwarabu na utwana ili watu waendele kuichukia Oman.)
Alisema vijana wengi wanaokutana na matatizo ya udhalilishaji ni wale wanaondoka kwa njia za panya bila ya kufuata taratibu za safari kutoka serikalini, hivyo kuwataka vijana kuhakikisha wanaondoka nchini kwa kufuata taratibu ili wanapopatwa na matatizo, serikali iwasaidie. (kwanza nyinyi mumeshindwa kuwajiri vijana,pili kunavijana wangapi walio hapo hapo Zanzibar munashindwa hata kuwapa mkate wa asubuhi na chai kavu wachilimbali kuwapa kazi mtaweza kuwasaidia walio anje ya nchi hebu wacheni kasumba na upumbavu kani mule haramu ya hiyo miaka mitano ikiwa m.mungu atawawacha muimalize musiwazidishe machungu watu kwa kubwabwaja kwenu kusiko na maana yoyote njia zapanya kila kijana anahaki ya kuwa na paspoti akitimia miaka 18 hamuwapi kwa uhasidi ulivyo waja mnatarajiwa wakae hapo wafe njaa..??)
“Ni kweli baadhi ya vijana hasa wanawake wanaokwenda kufanya kazi za ndani Oman na Muscat, huwa wanafanyiwa vitendo vya udhalilishaji na waajiri wao huwanyang’anya hati za kusafiria ili wasiweze kurudi wanapodhalilishwa. ”(nyinyi na MAZOMBI wenu mushawadhalilisha wanawawake wa kizanzibari mara ngapi...?)
Aidha, alisema licha ya kudhalilishwa na kunyanyaswa kijinsia, alisema vijana kutoka Zanzibar ni wavivu wa kufanya kazi na kuwapa wakati mgumu waajiri wao. (wavivu wavivu lini serikali lenu la kijambazi liliwapa kazi wasichana wa kizanzibari wakafanya uvivu...? wewe Mzambi umekimbia kwenu umekuja hapa umekuwa waziri unakula mshahara wabure wa kodi za hao hao unao waita wavivu ambao mumewavunjia mabanda yao,mamatilie,kina dada wauza chapati ndio unakula kodi zao kisha unawaita wavivu mbwa mkubwa wee utarudi zambia ukalime mahindi subiri tu.)
Alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Kampuni za Uwakala wa Ajira Zanzibar, imewaunganisha vijana 498 kwenda kufanya kazi Oman, Qatar, Kuwait na Saudi Arabia. (simnasema warabu watu wabaya sasa kwanini serikali lenu la kijambazi halianzishi kazi hapo hapo zanzibar mukawajiri mummo tu kuwapeleka huko huko kwa warabu munavyo waita nyinyi masultani kwa nini....?)
Alisema vijana hao wameajiriwa kwa nafasi za kazi za udereva, saluni, hoteli, upishi, kazi za nyumbani, ubaharia, taasisi za fedha, viwandani na ulinzi katika sekta binafsi. (OH Zanzibar si tuliajiri wenyewe hapa kisha nyinyi mkasema marufuku kufutarisha kuuza chakula, chips mishkaki, urojo, juice, hata kahawa, serikali inawavunjiya wafanya biashara sehemu zao za kutafuta risk. Acheni undumi la kuwili kama hamna hoja kakayeni maskani ya kisonge mcheze bao.
Hata hivyo, alisema bado kuna wimbi kubwa la vijana wa Zanzibar ambao hawana ajira pamoja na juhudi za serikali za kuwajengea uwezo wa kujiajiri kupitia sekta isiyo rasmi. Castico alisema serikali chini ya mpango huo, imefanikiwa kutoa mikopo 337 yenye thamani ya Sh. milioni 523.4 na kuwanufaisha wananchi 1,907 Unguja na Pemba. (Kama serikali ya madikteta uchwara ya Tanganyika na Zanzibar imeshindwa kuwapa ajira wananchi na sasa mnajidai ati kutoa mikopo nyinyi wenyewe mishahara yenu ni ya kubangaiza mtawapa rai mikopo porojoo tu semeni kweli munawapa watu wa maskani za CCM hapo tutakubali lakini sio wananchi.)

RAIS WA NYOYO ZA WATU KAUKATA MKONO WA BABUALI KATAKATA


13934693_1422159237810536_6365789940294090635_n

BAADA YA MAALIM SEIF SHARIFF HAMAD RAIS WA NYOYO ZA WAZANZUBARI KUMNYIMA MKONO HUYU KIBARAKA WA WAKOLONI WEUSI TANGANYIKA ANAE TUMIWA KUIMALIZA ZANZIBAR NA WAZANZIBARI MUUNGALIE USO WAKE ULIVYO POROMOKA HIYO NI DUNIA TU MZEE KARUME KENDA MZEE JUMBE HUYO ASHAKWENDA NA WEWE SHEIN NA SISI PIA TUTAKWENDA JIANDAE UTAMJIBU NINI MWANYEZI MUNGU HUKO HAKUNA MAZOMBI WALA JESHI WALA POLISI UMEBEBA DHIMA KUBWA SANA UMEDHULUMU NCHI NZIMA KWA RAHA YA SEKUNDE TU.


Salamu hizi zikufikie wewe Naibu Waziri wa Fedha wa zamani wa Serikali ya Muungano Abdulsalam Isssa Khatibu Mzee Jumbe M.Mungu amsamehe na ampe malazi mema peponi Ameen, alikuwa na Baraza la Mapinduzi, Baraza la Mawaziri na Baraza la Wawakilishi, alikuwa na wanasheria mahiri akina Daurado, kwa nini alijifungia peke yake kupanga mpango wa kudai nchi ya Zanzibar yenye mamlaka kamili peke yake....?? Mulisikia wapi au ulimwengu gani mtu moja ati akadai nchi....?? Mfano hai huwo hapo Maalim Seif anadai nchi ya Zanzibar anaidai peke yake.....??
Lengo lake halikuwa na manufaa kwa nchi ya Zanzibar. Tayari alishaanza mikakati ya kibaguzi dhidi ya Wapemba. Alikuwa anaandaa sera za “Revolutionary Justice”. Yaani sharia za kimapinduzi kama ilivyokuwa wakati wa Karume baada ya mapinduzi ya 1964. Najuwa tayari kuna Watu bado Wanasema Kwamba Maalim Sefu ndie aliemsaliti Mzee Jumbe, kinachonishangaza hawa wanaosema hivo Kwanini Hawataki kukisoma Kitabu kilichoandikwa ” The Memour Of Sef Sharif Hamad & Ali Sultan Issa”?
Kitabu kilitoka zamani sana tokea Mzee Jumbe yuko hai na anafahamu zake, kama yale alioeleza maalim Sefu Sharifu Hamadi mule ndani ya Kitabu hicho Kuhusu Mzee Aboud Jumbe na Mpango wake Wakujivua ktk Muungano Ili Awameze Wanasiasa Vijana wenye asili ya Pemba. Yeye Mzee Jumbe ana copy ya hicho kitabu na mbona hajajitokeza kwenye Media na Kukanusha kama aliosema maalim Sefu ni Uwongo…?? Nashangaa inakuja MIHAFIDHINA , Midgalimu Leo hii na tokea hapo Nyuma na kufumbua Midomo yao inayo nuka nakusema ..Oooooh maalim Kamsaliti Mzee Jumbe.. Thut is “NON SENS”
Ukweli nikwamba katika baraza la Mapinduzi Kulikuwa na Members kama hao Kina Mzee Moyo,Generel Yussuf Himid, Kisasi, na wengine . Walichukizwa na kuona Mzee Jumbe ametowa nafasi za kusomesha Vijana Wapya wa Kizanzibari hasa wenye asili ya Kipemba kwa wakati ulee. Na Argument yao ilikuwa nikwamba Wapemba Hawakupinduwa.. Well is better said the truth, kwamba yaliofanywa 12-1.1964 hayakuwa Mapinduzi bali ni Mauwaji ya Waislamu dhidi ya Waislamu wenye asili mbali mbali.
Hivo hizo Serikali 3 za Mzee Abudu Jumbe hazikuwa na maana yoyote kwa wakati huo dhidi ya jamii fulani , ila kuzidisha vugu vugu la maonevu na mauwaji ya kinyama kama waliofanyiwa Akina. Abdallah Kassim Hanga, Mdungi Ussi, Othman Sharif na wengine wengi sana sana walio uliwa na kufanywa kila aina ya machafu. Hizo ndizo Serikali 3 zilizokuwa zikitafutwa na Mzee Abudu Jumbe pamoja na kundi lake la Yusuf Himid na Hassan Nassor Moyo..enzi zileeee.
Na maalim Sefu hakuwa katika Member wa baraza la Mapinduzi wala hakuwa Close na Rais Mzee Abudu Jumbe. Hivo ilikuwa taabu kuona nyaraka zake za Siri. Nyaraka zilitolewa na Wahafidhuna Wa Kiunguja ambao ndio waliokuwa karibu na Raisi. Vyereje Mpemba awekwe Close na Raisi wakati Mikono yake haina Damu ( so call Mapinduzi) ? Sasa mbona kama muna mashaka na ukweli huo hamwendi mukauliza kwa hao wanamapinduzi waliobakia?..Au Ndio munawaona hawana akili..??
Sasa huyo Abdulsalami Issa naache Unafiki Wake na chuki zake dhidi ya Maalim Sefu. Naaseme Ukweli uliokuwepo. kama hajuwi Kusoma naamini ana watoto wake kawasomesha nje na wengine wako Nje wanaishi.. na wamnunulie kitabu wamsomee ukweli........

Tuesday, August 16, 2016

VIDEO-BALOZI SEFU ALIUTUMIA VIBAYA MDOMO WAKE.



Balozi Sefu yuko nchini India kwa ajili ya matibabu na safari hii ya India imekuja baada ya magonjwa yake kushindikana nchini CUBA ambako inasemekana alienda pia kwa ajili ya matibabu.

Sote tunakumbuka Balizi Sefu alivyoutumia mdomo wake kuwadhalilisha hadharani mashehe wa Uamsho huku akijisifia kwa kusema kua wananyea ndooni. Pia Balozi Sefu alisikika akimwita Maalim Seif bwege na kuahidi kua wao wataendelea kumpiga kwa vile kiongozi huyo ni bwege.

Haya yote Balozi Sefu aliyasema akitumia mdomo wake na kusistiza kwa mkono wake wa kulia huku akisahau kua dua za mwenye kudhulumiwa (Wazanzibari) M/Mungu hawezi kuzipuuza. Hatimae Balozi sasa yanayomfika anamtafta mchawi wakati mchawi ni yeye mwenyewe.

Balozi Sefu mdomo wake umepinda sasa na zipo taarifa kua anatumia zaidi mkono wa kushoto baada ya mkono wake wa kulia kupata stroke na kupungua nguvu. Pia Balozi Seif anatazamiwa kua huenda akapoteza nafasi yake ya umakamo wa pili kutokana na hali yake ya afya kuzidi kua mbaya.

Wako wanasema kua Balozi Sefu haumwi na chochote lakini bila ya shaka hawa ni wale wanaosubiri kuskia yuko mahututi au waskie taarifa kutoka katika Serikali yao haramu au chanzo chao cha habari cha CCM (ZBC)ndipo waamini jambo ambalo ni kugumu sana kutokea.

Sisi tunayasema haya na kuwathubitishia kwa picha sasa mwenye macho ataona na mwenye maskio bila ya shaka muda ukifika ataskia.

# ZANZIBAR NI NJEMA ATAKAE AJE #

Thursday, August 11, 2016

WATANGANYIKA WANAKUFURU NA KUSEMA POMBE MAGUFULI KALETWA NA MUNGU JE NYERERE,MWINYI,MKAPA NA KIKWETE WALILETWA NA NANI AU SHETANI.....??


Afbeeldingsresultaat voor magufuli

Bila kutafuta namna ya kutafuna maneno kwa kuhofia au kupenda leo nimeona iko haja ya kuwa fahamisha wanaoitwa ndugu zetu iwe wa damu, kweli au kisiasa tu, ni vema sasa Watanganyika wakaelewa kuwa sisi ndugu zao wa visiwani tunaoaminishwa kuwa tumehusiana japo kuwa uhusiano huo hauwazuwii wao kututawala kwa mabavu na sisi kujipendekeza kwa kiu ya kuto kukoma kutawaliwa bila huruma huku nguvu za vyombo vya dola vikitumika kuisidikiza na kuisimika demokrasia bila ridhaa ya wahusika walio wengi,kama sio mtu mweusi tena mpinduzi na sio chotara au Muarabu kabisa haya yanayo tendeka kwetu na yanayo kuja Tanganyika huwezi kuyaelewa wala kuyapa baraka zako hata uwe na elimu ya shahada ya mwisho hiyo haitokusaidia kufikiri labda kukupa ajira pekee katika moja ya idara,mashirika na wizara za mapinduzi iwe katika chama au sirikali.
Tanganyika wakitaka wasitake na wao tayari wamesha pata kiongozi kama wale tulio wazowea huku kwetu ambao siku zote hawa heshimu maamuzi ya raia au wananchi,ni vema nikawa mkweli viongozi wetu hao au hawa hawana sababu ya kuheshimu chochote kutoka kwa waungwana sisi kwa sababu ikiwa hatukuwachagua na wanajua kuwa wamewekwa na kujiweka kwa nguvu za mitutu waliyo washikisha wajukuu zao sasa wana deni gani kwetu? Mtawala mpya wa Tanganyika Bwana au Chifu Magufuli tangu aingie katika Usultani ameshindwa kujizuwia kutawala kwa kutumia “MDOMO” wake mtupu, katiba na sheria hakuwahi kuzisikia yeye amejikita katika kutoa amri pekee tena nyingi za ovyo “decree” kila kinacho toka mdomoni mwake ndio sheria hata wanao tawaliwa wamefika kukufuru na kudai kinatoka kwa Mungu, na Mtawala huyu ameletwa na Muumba huyo huyo,sasa la kujiuliza wale kina Mwinyi,Nyerere,Kikwete na Mkapa waliletwa na CCM peke yake? au shetani alihusika na ujio huo?
Huku ni kuchangayikiwa mimi sithubutu kushtuka na kauli za aina hii kwa sababu Watanganyika juu ya kuwa ni weledi wa kutuzulumu na kututawala kwa zaidi ya miaka hamsini lakini viumbe hawa wana kasoro nyingi za kibinaadamu kama tulizo nazo sisi,huyu Magufuli hakuwa chaguo lao wengi walimtaka Lowassa,Membe na Amina katika halmashauri kuu ya chama chetu lakini baada ya mchezo kama ule wa karata wa mzungu kalala wapi, wote wakajikuta wamaimba nyimbo za kisukuma bila kutaka sasa wanatakiwa wacheze na ngoma za asili,kimila za kabila hilo hilo wameanza kugoma na kumlaani Kiongozi huyu anae wafagilisha ovyo kila jumamosi kwa nguvu, sasa nani hapa alaumiwe kwa mtukufu huyu mlie dai kaletwa na YESU.
Mtukufu mtawala wa Tangayika bila hofu wala woga ametangaza kuvipiga maraufuku vyama vya siasa kuacha kufanya kazi hiyo eti kwa kuwa ana hitaji nafasi ya kuwaletea maendeleo, na baada ya miaka mitano ndio apimwe kama anafaa au hafai, la kushangaza hapa nani kampa madaraka makubwa kama haya ya kubadili katiba ya nchi,kauli yake sio sheria wala haiwezi kuwa hivyo katika nchi yoyote yenye watu wenye akili timamu, ni lazima Watanganyika wawe wanaugua maradhi yoyote labda “amnisia”/ kusahau ovyo ovyo, ndio waruhusu amri kama hizi za kipumbavu kutukika,nimeziita za kipumbavu kwa sababu sina neno jingine sahihi,lakini pia ni lazima mimi kama Mzanzibari au Mtanzania ninae amini haki,umoja na usawa katika Muungano huu kuwatakia kila wanalo stahiki/ adhabu Watanganyika katika kipindi hiki cha utawala wa mtukufu wao, kwa sababu wao ndio kisa au msiba wa uhuru na maisha yetu.
Uungwana wangu haunizuwii kudai kisasi hasa kwa kuwa hata dini yangu imetowa baraka zake katika hili.Watanganyika mmetutesa na manaendelea kututesa kila kukicha kwa kusaidiana na hawa waislamu wenzetu hapa waliopo katika serekali yenu, sasa na nyie zamu yenu kuonja madhila ya kutawaliwa na watu au mtu mnae mjua kuwa mwenzenu lakini kumbe ni adui yenu na ataendelea kuwa hivyo siku zote mpaka pale mtakapo itafuta dawa ya kukabiliana nae.
Niliwahi kusema huko nyuma kuwa Zanzibar inaigharimu Tanganyika siku zote,kuitawala haijawahi kuwa tatizo kwa Tanganyika, tatizo ni kiasi gani Tanganyika itaelewa na kufahamu kuwa gharama wanayo ipata siku zote kwa kuikumbatia Zanzibar kwa mabavu itaimaliza kwa kuisambaratisha Tanganyika na mwisho wake Zanzibar itakuwa huru na Tanganyika itabakia vipande vipande, sasa kwa kasi ya Mtawala wenu bwana hapa kazi tu, huyu aliebatizwa jina la dikteta uchwara ambalo kwa kweli Tundu Lissu hakukosea kwa kuwa Magufuli hawezi kuwa Kagame kama vile Iddi Amini hakuweza kuwa Hitler, Tanganyika endeleeni kuitawala zanzibar lakini mkumbuke kuwa South Sudan inawapigia hodi.
Nawashukuru WAZANZIBARI WOTE/ NA kuwasalimia Watanganyika.

VIDEO-SALAMU ZENU MNAO WAPA MAJINA MABAYA MASHEIKH WETU NA NDUGU ZETU

IN AMERICA
IN GERMANY
IN INDIA


mant2

mant3

mant1

Tuesday, August 9, 2016

RAIS MAGUFULI NI DIKTETA UCHWARA......???


YASOME MAONI YA PROFESA JOSEPH MBELE KUHUSU KAULI ZA TUNDU LISSU
RAIS MAGUFULI NI DIKTETA UCHWARA?
Na Profesa Joseph Mbele
Nimeona nianzishe mjadala wa suala linalovuma wakati huu nchini Tanzania, ambalo ni: Je, Rais Magufuli ni dikteta uchwara...?
Tundu Lissu, mwanasheria wa CHADEMA ndiye mwanzilishi wa dhana hii ya kwamba Rais Magufuli ni dikteta uchwara. Kwa kuanzia, ninapenda kuwashutumu polisi na watawala wa CCM kwa namna walivyolishughulikia suala hili.
Kwa mujibu wa katiba ya Tanzania, Tundu Lissu ana haki na uhuru wa kuwa na mawazo yake kuhusu suala lolote. Ana haki na uhuru wa kuwa na mtazamo wake juu ya Rais Magufuli. Ana haki na uhuru wa kutoa mawazo yake kama alivyofanya.
Mtu mwingine yeyote naye ana haki na uhuru huo. Kwa hivi, kauli ya Tundu Lissu haikuhitaji hatua zilizochukuliwa na polisi za kwenda kumkamata na kumsafirisha kutoka Singida hadi Dar es Salaam kwa mahojiano makao makuu ya polisi.
Jambo ambalo lingeweza kufanyika, bila taabu yote hii na ufujaji wa hela za walipa kodi, ilikuwa ni kwa serikali kujibu hoja za Tundu Lissu na kuthibitisha kuwa Rais Magufuli si dikteta uchwara. Malumbano ya hoja yangetosha.
Ndio utaratibu unaotakiwa katika jamii iliyostaarabika. Ninaamini kuwa wa-Tanzania wana akili timamu, na wana uwezo wa kuchambua mambo. Wana uwezo wa kusikiliza hoja za pande mbali mbali na kutambua upande upi ni sahihi. Madai ya polisi na watawala wa Tanzania kwamba kauli ya Tundu Lissu ni uchochezi ni ya kuwadhalilisha wananchi. Ni kusema kwamba wananchi ni wajinga, wasio na uwezo wa kutathmini na kuchambua mambo.
Ni kwa nini serikali haikuchukua njia hii ya kujibu hoja kwa hoja? Inamaanisha kwamba katika serikali nzima hakuna mtu mwenye akili ya kuweza kumpinga Tundu Lissu na kuthibitisha kuwa Rais Magufuli si dikteta uchwara...? Inamaanisha kuwa watendaji wote wa serikali hii ya CCM ni watendaji uchwara, au ni watendaji hewa, au ni vilaza...?
Rais Magufuli, kwa mtazamo wangu, amekuwa akivuka mipaka ya katiba kwa baadhi ya kauli zake. Hana mamlaka kikatiba wala kwa mujibu wa sheria za vyama vya siasa, kuweka vizuizi juu ya mikutano na maandamano ya vyama vya siasa. Taratibu zote zimeelezwa katika katiba ya Tanzania na katika sheria ya vyama vya siasa.
Kwa bahati nzuri, katiba ninayo na nimeisoma, na sheria ya vyama vya siasa, ambayo imewekwa kwenye tovuti ya ofisi ya msajili wa vyama, nimeisoma pia: http://www.orpp.go.tz/en/rules/. Kwa kupitia katiba na sheria, ni wazi kuwa Rais Magufuli anakiuka katiba na sheria, na kwa hivyo, kauli ya Tundu Lissu kwamba Rais Magufuli ni dikteta uchwara ni sahihi.
Vyama vya siasa vinawajibika kufanya mikutano na maandamo kwa amani, ili kutangaza sera zao, kutafuta wanachama wapya, na kadhalika. Rais Magufuli, au mtu mwingine yeyote hana wadhifa wa kuwawekea zuio kama alivyofanya. Hana mamlaka ya kusema kwamba watu wafanye siasa katika maeneo yao tu. Hana mamlaka ya kutangaza, hata kwa kisingizio cha "hapa kazi tu," shughuli zipi za kisiasa zisitishwe hadi mwaka 2020. Huu ni udikteta.
Mimi ni raia ambaye si mwanachama wa chama chochote cha siasa. Ninachotaka ni kuona nchi inaendeshwa kwa mujibu wa katiba na sheria zilizopo. Ninataka utawala wa sheria, unaozingatia haki za binadamu.

NCHI HII INAVIWANDA VYA KUKAMULIA MAJI DUUUUH!!!

TUMEJIPANGA MWAKA HUU WATAISOMA UKISHA KUCHEZA MIJASHO
ISHAKUTOKA UNANUKA MAKWAPA UKIRUDI NYUMBA HUNA HATA
MAJI YA KUPIGIA MSWAKI WACHILIAMBALI KUOGA ILIO BAKI NDIO 
KWENDA KUJIPANGA SASA FOLENI YA MAJI WAKATI WAO VIONGOZI
WA CCM WANAMAJUMBA ZAIDI YA MATANO NA YOTE YANA MAJI NA UMEME
NYINYI MUMO TUUU TUMEJAPANGA MWAKA HUU WATAISOMA NDIO MUNAISOMA SASA



Serikali ya viwanda...naona wakina mama huko Katoro Geita wakiwa kwenye kiwanda cha kukamua maji
😂😂😂😂
Toka enzi za Babu na Bibi mnahaidiwa maji mpaka leo na bado hamtii akili,mkaichagua CCM kwa mbwembwe,,,na iwe fundisho na bado mtakunywa hadi matope.
Hawa ndio walisemaga "mabadiliko mpelekee kinyonga" leo wao ndio wanageuka vinyonga wananyonga kiwanda cha maji kwa mbaali,,,ama kweli shetani afukuzwi kwa ubani.

Monday, August 8, 2016

TAFADHALI TAFADHALI YOYOTE ANAE MJUWA HUYU DADA AWAPE HABARI JAMAA ZAKE KUWA AMEFARIKI HUKO OMAN


Inallilah waina lilahi rajiuni ,mungu ailaze roho yake mahala pema peponi,uyu dada alikufa Omani leo ni siku ya tatu yuko mochari na dhani kuwa familia yake ina habari , tusaidianeni kusambaza picha hii ndugu waislam na hata wasio waislam ,ama kama kuna mtu anae mfahamu vzr atambulishe familia yake, baada ya ayo, Asalam alaikum warahtullah wabarakatus — feeling sad at Al Qassim.

HII NDIO HISTORIA YA UKWELI YA NCHI YA TANGANYIKA KABLA YA KUVA KOTI LA TANZANIA NA KULAZIMISHA KUIMEZA NCHI ZANZIBAR NA KUIFUTA HISTORIA YA KWELI YA TANGANYIKA.

PART 1
PART 2
PART 3
PART 1
PART 2
PART 3

Sunday, August 7, 2016

TUNDU LISSU A.K.A RONALDO HAJAWAHI KUJARIBIWA KATIKA SHERIA NA HATOJARIBIWA NA MKIMJARIBU ATAWAUBUWA


Lissu hajawahi kujaribiwa katika Sheria. Na hatojaribiwa. Hata refarii utoe macho vp jamhuri ndo ishapigwa hivyo. Usimjaribu tena. Utaambulia aibu nyingine. Nasema Lissu hajaribiwi na hatajaribiwa.!


DUBAI YA SHEIN HIYOOOOOO

DUBAI YA SHEIN HIYOOOOOO

Saturday, August 6, 2016

TUNDU LISSU A.K.A. RONALDO AIBUWA MTIKISIKO WA AINA YAKE KATIKA MAHAKAMA ZA HAKIMU MKAZI KISUTU


Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria wa CHADEMA, Tundu Lissu, aliibua mtikisiko wa aina yake katika viunga vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dsm jana wakati alipofikishwa kukabiliana na tuhuma atii za uchochezi. Baada ya kupandishwa kizimbani na kusomewa mashitaka yake, ubishani mkali wa kisheria uliibuka na kudumu hadi giza lilipoingia mishale ya saa 2:25 usiku, ikiwa ni moja wapo ya kesi nadra za aina hiyo kunguruma hadi usiku. Lissu alikamilisha taratibu za kujidhamini mwenyewe saa 2:56 usiku baada ya kutimiza masharti kadhaa likiwamo la kusaini hati ya dhamana yenye thamani ya Sh. milioni 10.