Saturday, December 17, 2016

MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA ACHA KUITAWALA ZANZIBAR KWA MITUTU WALISHINDWA MAKABURU MTAWEZA NYINYI MAKABURU WEUSI CHAMA CHA MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA CCM CHA CHANGANYA DINI NA SIASA KISIWANI PEMBA NCHINI ZANZIBAR

Afbeeldingsresultaat voor mabomu na risasi pemba
Afbeeldingsresultaat voor mabomu na risasi pemba
Afbeeldingsresultaat voor mabomu na risasi pemba
Risasi na mabomu yaridima nchini zanzibar kisiwani pemba.

Ugomvi mkubwa umezuka kutokana na kutajwa Shein Kitumwa cha Mkoloni Mweusi Tanganyika katika khutba ya ijuma. Imamu wa Msikiti ambae ni CCM alifanya hivyo mbona CCM mnachanganya Dini na Siasa......? na wananchi wa pemba hawakukubali kitendo hicho kifanyike. Msikiti ulichomwa moto na watu wanaosadikiwa kuwa ni Usalama wa Taifa kwa makusudi ili kuchochea zaidi na lengo lao ni kusingizia wananchi waishio pemba ambao karibia wote ni Wapenzi wa Chama Cha CUF ili waweze kupata sababu ya kuwapiga na kuwafunga jela dikteta shein anaonyesha wazi kuwa siasa imemshinda na sasa anatafuta kilasababu aichafuwe nchi iwe haikaliki akishirikiana na Mkoloni Mweusi Tanganyika.

Milio ya risasi na mabomu yamekuwa yakisikika huko Kangagani kisiwa Pemba nchini Zanzibar. Hali hii imewafanya wakazi wa Kangagani usiku wajana kuamkia leo kuyakimbia majumba yao na kukimbia misituni kupata manusura. Chanzo na Kisa cha kufanya Wananchi wote hawa wasiweze kulala katika majumba yao na kuishia kulala maporini na misituni ni kukata na kupinga jina la Dikteta Shein lisitanjwe kwenye Khutba ya Ijumaa tunawauliza tena CCM mbona mnachanganya Dini na Siasa...? 

Tokea mchana wakati wa Swala ya Ijumaa hali imekuwa tete kwa wakati wa Kangagani kisiwani Pemba nchini Zanzibar ambapo waliswali Ijumaa chini ya ulinzi mkali wa jeshi la Mkoloni Mweusi Tanganyika na Mitutu yao na Mabomu ya Machozi huku Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini na Mkuu wa Wilaya ya Wete walio wekwa na Mkoloni Mweusi Tanganyika na sio kwa kura za Wananchi wote wakiwa wamehudhuria. Wiki iliyopita vijana 7 wamekamatwa na polisi hadi leo hii wako mahabusu.
Bado haijajulikana wa watu wangapi mpaka sasa wameumia kwenye Mashambulizi haya ya jeshi la Mkoloni Mweusi Tanganyika la kuwashambulia Wananchi wa Nchi ya Zanzibar hapa Kangagani kisiwani Pemba, lakini inasemekana majeruhi ni wengi.Pia haijajulikana mpaka sasa ni watu wangapi wamekamatwa.

No comments:

Post a Comment